Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya vijito, unaozaa matunda kwa wakati wake, na majani yake hayanyauki hata kidogo. Anafanikiwa katika yote anayofanya.
Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.
na kuwapa wale wanaoomboleza katika Sayuni taji la maua pahali pa majivu juu ya kichwa, mafuta ya kuangarisha kwa furaha pahali pa maombolezo, nguo ya sifa pahali pa moyo muzito. Nao wataitwa miti ya mialo ya haki, Yawe aliyopanda kuonyesha utukufu wake.
Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya maji, unaopenyeza mizizi yake karibu na chemichemi. Hauogopi wakati wa jua kali, majani yake yanabaki mabichi. Hauhangaiki katika mwaka wa ukosefu wa mvua, nao haukosi kuzaa matunda.
Hii ni hukumu iliyotangazwa na walinzi; ni uamuzi wa wanaokuwa watakatifu, kusudi wanadamu wote kila pahali wapate kutambua kwamba Mungu Mukubwa ana mamlaka juu ya falme zote za wanadamu; yeye anamupatia ufalme mutu yeyote anayemupenda, anamufanya kuwa mufalme hata mutu muzaifu wa mwisho.
Akaona muti wa tini pembeni ya njia, akaenda karibu nao, lakini hakuona kitu juu yake isipokuwa majani matupu. Halafu Yesu akaulaani muti ule akisema: “Wewe usitoe tena matunda tangu leo hata milele!” Na pale pale muti ule ukakauka.
Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?