“Kweli ninawaambia: kati ya watu wanaoishi katika dunia, hakuna mutu anayekuwa mukubwa kuliko Yoane Mubatizaji. Lakini yeyote anayeonekana kuwa mudogo katika Ufalme wa mbinguni anahesabiwa kuwa mukubwa kuliko yeye.
Wale wanafunzi wa Yoane walipoondoka, Yesu akaanza kuwaambia makundi ya watu habari za Yoane: “Mulienda katika jangwa kwa kuangalia nini? Tete linalotikiswa na upepo? Hapana!
Nao wakamujibu: “Wamoja wanasema kwamba yeye ni Yoane Mubatizaji; wengine wanasema kwamba yeye ni Elia, na wengine wanasema ni Yeremia au mumoja wa manabii wengine.”
Kwa maana Yoane alikuja kwenu kuwaonyesha njia ya haki, nanyi hamukumusadiki. Lakini walipishaji wa kodi na makahaba walimusadiki. Na ijapokuwa muliona mambo hayo yote, hamukugeuka toka zambi zenu na kumusadiki.”
Wale wajumbe wa Yoane walipokwisha kuondoka, Yesu akaanza kuwaambia makundi ya watu habari za Yoane akisema: “Mulienda katika jangwa kuangalia nini? Tete linalotikiswa na upepo? Hapana!
Lakini sasa ni muda wa miaka makumi ine na mitano tangu Yawe aliposema na Musa, wakati Waisraeli walipokuwa wanapita katika jangwa. Tangu wakati ule Yawe, kama vile alivyoahidi, amenilinda muzima mpaka leo, na sasa mimi nina umri wa miaka makumi nane na mitano.
Wazao wa Keni ambaye alikuwa baba mukwe wa Musa, walifuatana na watu wa kabila la Yuda kutokea Muji wa Miti ya Ngazi, ni kusema muji wa Yeriko, mpaka jangwa la Yuda karibu na Aradi, wakafanya makao yao kule pamoja na watu wa Yuda.