Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 28:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Mara moja Yesu akakutana na wale wanawake, akawasalimia. Wakajongea karibu naye, wakamushika miguu na kumwabudu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 28:9
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sisi wote tumekuwa kama watu wachafu; matendo yetu yote mema ni kama nguo chafu. Wote tunanyauka kama majani, uovu wetu unatupeperusha kama upepo.


Basi wanafunzi waliokuwa ndani ya chombo wakapiga magoti mbele ya Yesu, wakisema: “Kweli wewe ni Mwana wa Mungu!”


Wanapenda vilevile kusalimiwa kwa heshima kwenye nafasi za makutano, na kuitwa ‘Mwalimu.’


Kisha Yesu akawaambia: “Musiogope, muende kuwaambia wandugu zangu waende Galilaya, na kule wataniona.”


Wakati walipomwona, wakamwabudu, lakini wamoja kati yao wakaona shaka.


Basi wale wanawake wakaondoka upesi kutoka kwenye kaburi, wakijazwa na woga na furaha kubwa vilevile. Wakakimbia kwenda kuwapasha wanafunzi wake habari ile.


Malaika akamufikia kwenye nyumba yao na kumwambia: “Salamu kwako, wewe uliyejaliwa neema kutoka kwa Mungu! Bwana yuko pamoja nawe.”


Nao walipokwisha kumwabudu, wakarudia Yerusalema wakifurahi sana.


Akakuja kuinama kwenye miguu ya Yesu, akilia. Machozi yake yakamwangika juu ya miguu ya Yesu, akaipanguza na nywele zake, akaibusu na kuipakaa marasi.


Halafu Maria akatwaa nusu ya litre ya marasi ya bei kali, yaliyotengenezwa na maua ya nardo safi. Akaipakaa kwa miguu ya Yesu na kuipanguza na nywele zake. Nyumba yote ikajaa harufu ya marasi.


Magaribi ya ile ile siku ya kwanza ya juma, wanafunzi walikusanyika katika nyumba na milango ilikuwa imefungwa, kwa sababu waliwaogopa wakubwa wa Wayuda. Mara moja Yesu akawatokea na kusimama katikati yao, akawaambia: “Amani kwenu!”


Toma akamujibu: “Bwana wangu na Mungu wangu!”


Basi kwa kumaliza, wandugu zangu, kwa heri. Mujikaze kuwa wakamilifu, mufarijiane ninyi kwa ninyi, mukuwe na nia moja, muishi katika amani, na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.


Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ