Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 28:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Yeye hayuko hapa: amefufuka sawa alivyosema. Mukuje, muone pahali walipolalisha maiti yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 28:6
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa maana, kama vile Yona alivyobaki ndani ya tumbo la samaki mukubwa kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku, ndivyo vilevile Mwana wa Mutu atakavyobaki ndani ya udongo kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.


Tangia wakati ule Yesu akaanza kuwaambia wanafunzi wake waziwazi kwamba ni sherti kwake kwenda Yerusalema, ateswe kule na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria, auawe, na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.


nao watamwua, lakini kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.” Halafu wanafunzi wakahuzunika sana.


Walipokuwa wakishuka toka kwa mulima, Yesu akawaamuru: “Musimwelezee mutu mambo muliyoona mpaka Mwana wa Mutu atakapofufuka.”


na kumutoa katika mikono ya watu wa mataifa mengine. Nao watamuchekelea, watamupiga fimbo na kumutundika juu ya musalaba. Lakini kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.”


na kumwambia: “Bwana, tunakumbuka kwamba wakati yule mudanganyifu alipokuwa angali muzima, alisema: ‘Kwa siku tatu kisha kufa kwangu, nitafufuka.’


Lakini kijana yule akawaambia: “Musishituke! Munamutafuta Yesu wa Nazareti aliyetundikwa juu ya musalaba. Yeye amefufuka, hayuko hapa. Muangalie, hapa ni pahali walipomuweka.


Kisha Yesu akaanza kuwafundisha wanafunzi wake, akisema: “Sherti Mwana wa Mutu ateswe na kukataliwa na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani pamoja na walimu wa Sheria. Atauawa na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake atafufuka.”


Lakini Petro alisimama, akaenda mbio mpaka kwenye kaburi. Alipoinama kuchungulia ndani yake, akaona tu vile vitambaa. Kisha akarudia kwake, akishangaa kwa ajili ya mambo yaliyotokea.


lakini hawakuona maiti yake. Basi wakarudia kutuelezea kwamba wamalaika waliwatokea na kuwaambia kwamba yeye ni muzima.


Kisha akawaambia: “Haya ndiyo maneno niliyowaambia wakati nilipokuwa ningali pamoja nanyi, kwamba sherti yatimizwe maneno yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Musa, katika maandiko ya manabii na katika Zaburi.”


“Baba ananipenda kwa sababu mimi mwenyewe ninajitoa kufa, kusudi nipate kuwa muzima tena.


Yesu akawajibu: “Mubomoe hekalu hili, nami nitalijenga katika siku tatu.”


Lakini Mungu alimufufua, akimufungua toka vifungo vya lufu, kwa sababu haikuwezekana afungwe na lufu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ