Matayo 28:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
2 Kwa rafla kukatokea tetemeko la inchi, kwa maana malaika wa Bwana alishuka toka mbinguni, akasukuma lile jiwe lililofunga kaburi pembeni na kuikaa juu yake.
Siku ya kwanza ya juma asubui mapema, kulipokuwa kungali giza, Maria wa Magdala akaenda kwenye kaburi. Alipofika kule akaona kama jiwe lililofunika kaburi limeondolewa.
Kwa rafla kukatokea tetemeko kubwa la inchi hata misingi ya nyumba ya kifungo ikatikisika. Na pale pale milango yote ikafunguka na minyororo ya wafungwa wote ikakatika.
Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.
Mungu aliwafunulia wale manabii kwamba ujumbe ule walioutangaza haukuwaelekea wao wenyewe, lakini uliwaelekea ninyi. Na sasa ujumbe ule umetangazwa kwenu na wale waliowahubiri Habari Njema kwa uwezo wa Roho Mutakatifu aliyetumwa toka mbinguni. Hata wamalaika vilevile wanatamani kujua mambo hayo.
Kisha hekalu la Mungu linalokuwa mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana ndani yake. Halafu kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi, tetemeko la inchi na mvua kubwa ya mawe.