Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 27:51 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

51 Na saa ile ile pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini. Inchi ikatetemeka, mawe makubwa yakapasuka,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 27:51
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Akatengeneza pazia kwa kitambaa cha kitani safi, cha rangi ya samawi, ya rangi nyekundu-nyeusi na nyekundu. Akalichora kwa michoro ya makerubi.


Aliwapiga waadui mishale yake, akawatawanya; alirusha umeme mukali, akawakimbiza.


Katika taabu yangu, nilimwita Yawe; nilimulilia Mungu wangu anisaidie. Toka katika hekalu lake, alisikia sauti yangu; kilio changu kilimufikia katika masikio yake.


Kisha akaweka lile Sanduku la Agano ndani ya hema na kutundika pazia, na kwa namna hiyo akafunika Sanduku la Agano, kama vile alivyoamuriwa na Yawe.


Katika mulima huuhuu, Yawe ataliondoa wingu la huzuni lililowafunika watu wote, kifuniko cha uchungu juu ya mataifa yote.


Akamwambia: Umwambie ndugu yako Haruni asiingie katika Pahali Patakatifu nyuma ya pazia wakati usiokubaliwa. Asiingie pahali pale maana ndipo nitakapotokea katika wingu juu ya kiti cha rehema. Asipotii, atakufa.


Lakini asilikaribie lile pazia wala ile mazabahu maana ana kilema, asipate kuchafua Pahali Patakatifu, kwa sababu mimi Yawe ndiye ninayewatakasa.


Milima ilikuona, ikanyauka; mafuriko ya maji yakapita mule. Vilindi vya bahari vilinguruma, na kurusha juu mawimbi yake.


Ulitoka kwenda kuwaokoa watu wako, kumwokoa yule uliyemusimika kwa kumupakaa mafuta. Ulimuponda mutawala wa jamii ya waovu, ukawaangamiza kabisa wafuasi wake.


Wakati wa kuvunja kambi, Haruni na wana wake wataingia katika hema, na kushusha pazia linalokuwa mbele ya Sanduku la Agano, kisha walifunike kwa pazia hilo.


Mukubwa wa waaskari na wale waliokuwa pamoja naye wakimuchunga Yesu walipoona tetemeko la inchi na mambo yote yaliyofanyika, wakaogopa sana, na kusema: “Hakika mutu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”


Kwa rafla kukatokea tetemeko la inchi, kwa maana malaika wa Bwana alishuka toka mbinguni, akasukuma lile jiwe lililofunga kaburi pembeni na kuikaa juu yake.


Basi pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini.


Mukubwa wa waaskari alipoona mambo yale yaliyotokea, akamusifu Mungu, akisema: “Hakika mutu huyu alikuwa mwenye haki!”


Tumaini hili linasimamisha imara na kulinda mioyo yetu kama vile nanga inavyosimamisha mashua imara. Nalo linapita katika pazia na kuingia katika Pahali Patakatifu Sana.


Na nyuma ya pazia lililotenga kile chumba cha kwanza, kulikuwa chumba kingine kilichoitwa Pahali Patakatifu Sana.


Na saa ile ile, kukatokea tetemeko kubwa la inchi, na sehemu moja ya kumi ya muji ikabomoka, na watu elfu saba wakakufa katika tetemeko lile. Watu waliobaki wakashikwa na hofu, nao wakamutukuza Mungu wa mbinguni.


Kisha hekalu la Mungu linalokuwa mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana ndani yake. Halafu kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi, tetemeko la inchi na mvua kubwa ya mawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ