Katika taabu yangu, nilimwita Yawe; nilimulilia Mungu wangu anisaidie. Toka katika hekalu lake, alisikia sauti yangu; kilio changu kilimufikia katika masikio yake.
Akamwambia: Umwambie ndugu yako Haruni asiingie katika Pahali Patakatifu nyuma ya pazia wakati usiokubaliwa. Asiingie pahali pale maana ndipo nitakapotokea katika wingu juu ya kiti cha rehema. Asipotii, atakufa.
Ulitoka kwenda kuwaokoa watu wako, kumwokoa yule uliyemusimika kwa kumupakaa mafuta. Ulimuponda mutawala wa jamii ya waovu, ukawaangamiza kabisa wafuasi wake.
Wakati wa kuvunja kambi, Haruni na wana wake wataingia katika hema, na kushusha pazia linalokuwa mbele ya Sanduku la Agano, kisha walifunike kwa pazia hilo.
Mukubwa wa waaskari na wale waliokuwa pamoja naye wakimuchunga Yesu walipoona tetemeko la inchi na mambo yote yaliyofanyika, wakaogopa sana, na kusema: “Hakika mutu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
Kwa rafla kukatokea tetemeko la inchi, kwa maana malaika wa Bwana alishuka toka mbinguni, akasukuma lile jiwe lililofunga kaburi pembeni na kuikaa juu yake.
Tumaini hili linasimamisha imara na kulinda mioyo yetu kama vile nanga inavyosimamisha mashua imara. Nalo linapita katika pazia na kuingia katika Pahali Patakatifu Sana.
Na saa ile ile, kukatokea tetemeko kubwa la inchi, na sehemu moja ya kumi ya muji ikabomoka, na watu elfu saba wakakufa katika tetemeko lile. Watu waliobaki wakashikwa na hofu, nao wakamutukuza Mungu wa mbinguni.
Kisha hekalu la Mungu linalokuwa mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana ndani yake. Halafu kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi, tetemeko la inchi na mvua kubwa ya mawe.