Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 27:41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

41 Vilevile wakubwa wa makuhani walimuchekelea pamoja na walimu wa Sheria na wasimamizi wa watu, wakisemezana hivi:

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 27:41
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Akiwachunguza, ninyi mutapona? Au munazani munaweza kumudanganya Mungu kama watu?


Uwaache hao wanaofurahia hasara yangu, washindwe wote na kufezeheka. Hao wote wanaojiona bora kuliko mimi, wapate haya na kufezeheka.


Basi, ninyi musikuwe na mazarau vifungo vyenu visipate kukazwa zaidi. Maana nimesikia kwamba Yawe wa majeshi amekusudia kuiangamiza inchi yote.


Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.


Kwa muda wa mwezi mumoja, nikaua wachungaji watatu wabaya. Tena uvumilivu wangu kwa kondoo ukaniishia, nao kwa upande wao, wakanichukia.


wakisema: “Wewe uliyetaka kubomoa hekalu na kujenga lingine katika siku tatu, ujiokoe sasa wewe mwenyewe! Kama wewe ni Mwana wa Mungu, ujishushe juu ya musalaba!”


“Aliokoa wengine, lakini sasa anashindwa kwa kujiokoa yeye mwenyewe! Yeye ni mufalme wa Waisraeli, sasa ajishushe pale juu ya musalaba kusudi nasi tupate kumwamini.


Maana atatolewa katika mikono ya watu wa mataifa mengine. Watamuchekelea, watamutukana na kumutemea mate.


Halafu Yesu akawaambia wakubwa wa makuhani, wakubwa wa walinzi wa hekalu na wazee waliokuja kumukamata: “Mumekuja na panga na magongo kama vile wanavyokwenda kukamata munyanganyi?


Watu walisimama pale wakiangalia. Nao wakubwa wa Wayuda walimusimanga Yesu, wakisema: “Aliokoa watu wengine, sasa ajiokoe yeye mwenyewe ikiwa yeye ndiye Masiya, yule aliyechaguliwa na Mungu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ