Kwa hiyo nitamugawanyia sehemu pamoja na wakubwa, atagawanya vitu vilivyotekwa pamoja na wenye nguvu. Alijitoa yeye mwenyewe hata kufa; aliwekwa kundi moja na watu wakosaji. Alizibeba zambi za watu wengi, akawaombea musamaha hao wakosaji.
Kwa maana ninawaambia, ni lazima yatimie kwangu maneno haya yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Naye alihesabiwa pamoja na watenda maovu.’ Kwa sababu yanayonielekea mimi yanafikia kwa mwisho wake.”