Wale watenda maovu wawili wakaikaa kwa kumushuhudia Naboti, kisha wakamushitaki mbele ya watu wote wakisema: “Naboti amemutukana Mungu na mufalme.” Basi, Naboti akapelekwa inje ya muji, akauawa kwa kutupiwa mawe.
ni kusema ngombe muzima aliyebakia atamupeleka na kumuteketeza inje ya kambi pahali safi ambapo majivu yanatupwa, naye atamuchoma kwa moto juu ya kuni. Atachomwa kwa moto pale pahali pa kumwangia majivu.
Kisha atamutwaa ngombe dume huyu na kumupeleka inje ya kambi na kumuteketeza kwa moto kama vile alivyofanya yule mwingine. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi ya jamii.
Ikiwa kuhani ambaye amepakwa mafuta ndiye aliyetenda zambi hata akawatia watu katika kosa, basi huyo atamutolea Yawe ngombe dume muchanga asiyekuwa na kilema akuwe sadaka kwa ajili ya zambi.
Mutu mumoja wa Kurene, aliyeitwa Simoni, baba ya Alesanduro na Rufu, alikuwa akipita katika njia, akitoka kwenye vijiji. Waaskari wakamushurutisha abebe musalaba wa Yesu.
Nao walipokuwa wakimupeleka Yesu kwenda kutundikwa, wakakutana na mutu mumoja aliyeitwa Simoni, wa inchi ya Kurene, aliyekuwa akitoka kwenye vijiji. Wakamulazimisha abebe musalaba wa Yesu na kumufuata nyuma.
Lakini kulitokea wanafunzi wengine, waliokuwa watu wa Kipuro na wa inchi ya Kurene, waliofika Antiokia. Nao wakaanza kusemezana na Wagriki vilevile, wakiwahubiri Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
Katika kanisa la Antiokia kulikuwa manabii na walimu wamoja. Kati yao kulikuwa Barnaba, Simoni aliyeitwa vilevile Nigeri; Lukio wa Kurene, Saulo na Manaeni, aliyekomaa pamoja na mufalme Herode.
Lakini kukatokea watu wamoja waliopingana na Stefano. Watu hawa walikuwa wa nyumba ya kuabudia iliyojulikana kwa jina la “Wenye Uhuru.” Nao walitoka katika inchi ya Kurene na ya Alesanduria, na kutoka jimbo la Kilikia na la Azia. Watu hawa wakaanza kubishana na Stefano