Na kulipokucha asubui mapema, wakamutosha Yesu kwa Kayafa na kumupeleka kwenye nyumba ya liwali. Lakini Wayuda wenyewe hawakuingia ndani ya nyumba ya liwali, kwa maana kwa njia ile wangejichafua na kutoweza kuwa tayari kula karamu ya Pasaka.
Yuda akatwaa kundi la waaskari pamoja na walinzi waliotumwa na wakubwa wa makuhani na Wafarisayo. Akakuja nao kwenye bustani wakibeba taa, mienge na silaha.
Walipokwisha kukamata mupango wa kutusafirisha kwa njia ya chombo mpaka Italia, wakamuweka Paulo na wafungwa wengine chini ya uangalizi wa mukubwa mumoja wa waaskari aliyeitwa Yulio. Yeye alikuwa wa kundi la waaskari lililoitwa “Kundi la waaskari wa mufalme.”