Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 27:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Pilato akawauliza tena: “Basi munataka nifanye nini na huyu Yesu anayeitwa Kristo?” Nao wote wakajibu: “Atundikwe juu ya musalaba!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 27:22
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watumishi wangu wote wanasema wazi, kila mugeni amekaribishwa katika nyumba yangu.


Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.


Kwa muda wa mwezi mumoja, nikaua wachungaji watatu wabaya. Tena uvumilivu wangu kwa kondoo ukaniishia, nao kwa upande wao, wakanichukia.


Nao watu walipokuwa wamekusanyika pamoja, Pilato akawauliza: “Munataka niwafungulie nani kati ya Baraba na Yesu anayeitwa Kristo?”


Liwali akawauliza: “Munataka niwafungulie nani kati ya watu hawa wawili?” Nao wakamujibu: “Utufungulie Baraba.”


Pilato akawauliza tena: “Yeye alifanya ubaya gani?” Lakini wakazidi kupiga kelele wakisema: “Atundikwe juu ya musalaba!”


Wakubwa wa makuhani na wakubwa wote wa Baraza Kubwa walitafuta mashitaki juu ya Yesu kusudi wapate kumwua, lakini hawakupata neno.


Mwanamuke yule akamwambia: “Ninajua kwamba Masiya anayeitwa Kristo, atakuja. Na wakati atakapokuja atatuelezea maneno yote.”


Ijapokuwa hawakupata sababu ya kumuhukumu kufa, wakamwomba Pilato awape ruhusa ya kumwua.


“Basi wandugu zangu, mujue hakika kwamba kwa njia ya huyo, habari ya kusamehewa zambi inahubiriwa kwenu. Na zaidi ya hii, hakuna mutu anayeweza kuhesabiwa haki katika mambo yote kwa njia ya kushika Sheria ya Musa. Lakini kila mutu anayemwamini anahesabiwa haki katika mambo yale.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ