Walipofika pahali ambapo Mungu alipomwagiza, Abrahamu akajenga mazabahu na kupanga kuni juu yake. Kisha akamufunga Isaka mwana wake na kumulalisha juu ya kuni kwenye mazabahu.
na kumutoa katika mikono ya watu wa mataifa mengine. Nao watamuchekelea, watamupiga fimbo na kumutundika juu ya musalaba. Lakini kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.”
Katika siku zile watu wamoja wakakuja kumwelezea Yesu habari juu ya wale watu wa Galilaya waliouawa na liwali Pilato walipokuwa wakichinja nyama za kutolea Mungu sadaka.
Basi wakaanza kumuvizia Yesu, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa kama watu wazuri kusudi wamunase katika masemi. Na kwa njia ile waweze kumutoa katika mikono ya watawala wa inchi.
Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Tiberio mufalme wa Roma, Pontio Pilato alikuwa liwali wa jimbo la Yudea, na Herode alikuwa mutawala wa jimbo la Galilaya na ndugu yake Filipo alikuwa mutawala wa inchi ya Iturea na ya Tarakoniti. Vilevile Lisania alikuwa mutawala wa inchi ya Abilene,
Na kulipokucha asubui mapema, wakamutosha Yesu kwa Kayafa na kumupeleka kwenye nyumba ya liwali. Lakini Wayuda wenyewe hawakuingia ndani ya nyumba ya liwali, kwa maana kwa njia ile wangejichafua na kutoweza kuwa tayari kula karamu ya Pasaka.
Usiku, mbele ya kutimia kwa siku Herode aliyotaka kumusambisha mbele ya watu, Petro alikuwa amelala ndani ya chumba katikati ya waaskari wawili. Alikuwa amefungwa na minyororo miwili, nao walinzi walikuwa wakichunga mulango wa kifungo.
Lakini walipokwisha kumufunga Paulo na kamba kusudi wamupige, yeye akamwambia jemadari mumoja aliyekuwa pale: “Sheria inawaruhusu kumupiga mwanainchi wa Roma, ingawa hajahukumiwa bado?”
Mara moja wale waliotaka kumusambisha kwa kumupiga fimbo wakamwacha. Yule mukubwa wa jeshi akaogopa alipotambua kwamba Paulo ni mwanainchi wa Roma, na kwamba alikuwa anamufunga na minyororo.
Kulipopita miaka miwili, Porkio Festo akamukomboa Feliki kama liwali. Na kwa sababu Feliki alitaka kujipendekeza kwa Wayuda, akamwacha Paulo katika kifungo.
Basi ni kwa sababu hii nimewaita kusudi tuonane na niseme nanyi, kwa maana ninafungwa na munyororo huu kwa ajili ya tumaini ambalo Waisraeli wanakuwa nalo.”
Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa babu zetu, ameonyesha kwamba mutumishi wake Yesu ni mwenye utukufu. Ninyi wenyewe mulimutoa na kumukana mbele ya mutawala Pilato, ijapokuwa Pilato alikuwa ameamua kwamba afunguliwe.
“Ndiyo, ni kweli mufalme Herode, naye mutawala Pontio Pilato walikusanyika katika muji huu pamoja na Waisraeli na watu wa mataifa mengine kwa kufanya shauri baya juu ya mutumishi wako mutakatifu Yesu, uliyemuchagua kuwa Kristo.
na kumwomba amwandikie barua za kumutambulisha katika nyumba za kuabudia za muji Damasiki. Katika barua hizo, Saulo alipewa ruhusa kwamba akiona watu wanaofuata Njia ya Bwana, ikiwa wanaume au wanawake, awafunge na kuwapeleka Yerusalema.
Muwakumbuke wale wanaofungwa, mukijisikia sawa vile wenye kufungwa pamoja nao. Vilevile muwakumbuke wale wanaoteswa, mukijisikia sawa vile wenye kuteswa kama wao.