Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 26:74 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

74 Halafu Petro akaanza kusema: “Nilaaniwe ikiwa ninasema uongo! Ninaapa kwamba simujui mutu huyu!” Na mara moja jogoo akawika,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 26:74
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Musiwaogope wale wanaoweza kuua tu mwili, lakini wasioweza kuua roho. Lakini zaidi mumwogope Mungu anayeweza kuharibu mwili pamoja na roho katika jehenamu.


Yesu akamujibu: “Kweli ninakuambia kwamba katika usiku huu, mbele jogoo hajawika utakuwa umenikana mara tatu.”


Nyuma kidogo, wale waliosimama pale, wakamufikia Petro na kumwambia: “Hakika wewe ni mumoja wao, kwa maana hata usemi wako unakutambulisha.”


naye Petro akakumbuka maneno yale Yesu aliyomwambia kwamba mbele jogoo hajawika, atakuwa amemukana mara tatu. Basi akatoka inje, akalia kwa uchungu sana.


Nao watu wote wakajibu: “Lazima ya damu ya mutu huyu ikuwe juu ya kichwa chetu na juu ya kichwa cha watoto wetu!”


Yesu akamujibu: “Kweli ninakuambia kwamba usiku huu, mbele jogoo hajawika mara mbili, utakuwa umenikana mara tatu.”


Lakini Petro akakana, akisema: “Sijui wala sifahamu maneno unayotaka kusema.” Kisha akatoka inje ya upango na kwenda kwenye kiingilio cha mulango. [Jogoo akawika.]


Lakini Petro akasema: “Sijui mambo unayoyasema.” Wakati ule alipokuwa angali akisema, jogoo akawika.


Lakini Petro akakana tena, na pale pale jogoo akawika.


Ingekuwa heri nilaaniwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya wandugu zangu wa damu,


Kama mutu hamupendi Bwana, alaaniwe! Bwana wetu, kuja!


Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.


Siku moja akamwambia mama yake: “Vile vikoroti vya feza elfu moja na mia moja ulivyoibiwa, nawe ukamulaani aliyekuiba nami nikiwa ninasikia, mimi niko navyo. Mimi ndiye niliyevibeba.” Mama yake akasema: “Mwana wangu ubarikiwe na Yawe.”


Lakini hatuwezi kuwatoa wabinti zetu wakuwe wake zao, maana tulikwisha kuapa kwamba mutu yeyote atakayemwoesha binti yake kwa mwanaume wa kabila la Benjamina alaaniwe.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ