Matayo 26:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
7 mwanamuke mumoja aliingia ndani ya nyumba, akiwa na chupa la jiwe lenye kuwa na marasi ya bei kali, akaimimia juu ya kichwa cha Yesu walipokuwa wakikula.
Wakati uleule nabii Elisha alimwita mumoja wa wanafunzi wa nabii, akamwambia: “Ujitayarishe kusafiri, twaa chupa hii ya mafuta, na kwenda Ramoti katika Gileadi.
Munajipakaa marasi na mafuta kwa wingi kisha munakwenda kumwabudu Moleki. Munawatuma wajumbe wenu huko na huko, kujitafutia miungu ya kuabudu; hata kuzimu walifika.
Yesu alikuwa Betania katika nyumba ya mutu aliyeitwa Simoni Mukoma. Walipokuwa wakikula, mwanamuke mumoja akaingia ndani ya nyumba. Alikuwa na chupa la jiwe lenye marasi ya bei kali yaliyotengenezwa na maua ya nardo safi. Kisha akavunja mudomo wa lile chupa na kumimia marasi juu ya kichwa cha Yesu.