Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 26:61 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

61 na kusema: “Mutu huyu alisema kwamba anaweza kubomoa hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa muda wa siku tatu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 26:61
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wao wakasema: “Utupitishe! Wewe ulikuja huku ukiwa mugeni na sasa unajifanya kuwa mwamuzi! Basi, tutakutendea mabaya zaidi ya wale wageni wako.” Halafu wakamusukuma Loti nyuma hata karibu wavunje mulango wake.


Uwaambie wamutie katika gereza na kumukulisha mukate kidogo na maji, mpaka nitakaporudi salama.”


Yehu aliporudi kwa wenzake, mumoja wao alimwuliza: “Kuna shida yoyote? Mwenda-wazimu huyu alitaka nini kwako?” Yehu akawajibu: “Si munamujua yeye na namna yake ya kusema?”


Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.


Alizarauliwa na kukataliwa na watu. Alikuwa mutu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mutu wa kuchukiza kwa watu; alizarauliwa na tukamwona si kitu.


Lakini wakati Wafarisayo waliposikia maneno yale, wakasema: “Ni Belzebuli, mukubwa wa pepo ndiye anayemupa mutu huyu uwezo wa kufukuza pepo.”


Kuhani Mukubwa akasimama na kumwuliza Yesu: “Haujibu hata neno? Watu hawa wanakushitakia nini?”


Petro alipotoka inje kwa mulango wa upango, mutumishi mwingine mwanamuke akamwona na kuwaambia wale waliokuwa pale: “Huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”


wakisema: “Wewe uliyetaka kubomoa hekalu na kujenga lingine katika siku tatu, ujiokoe sasa wewe mwenyewe! Kama wewe ni Mwana wa Mungu, ujishushe juu ya musalaba!”


Yuda akatupa vile vikoroti ndani ya hekalu, naye akaondoka na kwenda kujitundika.


“Sisi tulimusikia akisema: ‘Mimi nitabomoa hekalu hili lililojengwa na watu, na katika siku tatu nitajenga lingine lisilojengwa na watu.’ ”


Watu waliokuwa wakipita pale walimutukana na kutikisatikisa vichwa vyao, wakisema: “Ewe! Wewe uliyetaka kubomoa hekalu na kujenga lingine katika siku tatu,


Wakaanza kumushitaki, wakisema: “Tulimukuta mutu huyu akiwashawishi watu wa taifa letu kufanya uasi. Yeye alikuwa akiwaambia kwamba wasilipe kodi kwa Mufalme wa Roma. Na zaidi ya hii anasema kwamba yeye ndiye Kristo, Mufalme aliyengojewa.”


Tunajua kwamba Mungu alisema na Musa, lakini hatujui pahali mutu yule anapotoka!”


Walimu wamoja wa kikundi cha Waepikurio na cha Wastoiko, wakaanza kubishana na Paulo. Wamoja wao wakauliza: “Huyu katetea anataka kusema nini?” Wengine wakasema: “Anaonekana kuwa muhubiri wa miungu ya kigeni.” Walisema hivi kwa sababu Paulo alikuwa akihubiri juu ya Yesu na jinsi alivyofufuka.


na kumushitaki: “Mutu huyu anawavuta watu kumwabudu Mungu kwa njia isiyopatana na Sheria yetu.”


Makutano walimusikiliza Paulo mpaka aliposema maneno yale. Kisha wakasema kwa nguvu: “Mumuteketeze mutu huyu! Mumwue, kwa maana hastahili kuishi!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ