Kapiteni wa mashua akamwendea, akamwambia: Namna gani wewe unaweza kulala? Amuka umwombe Mungu wako; labda Mungu wako atatuhurumia na kuyaokoa maisha yetu.
Akawaacha tena kwa mara ya pili, akaomba akisema: “Ee Baba yangu, kama kikombe hiki cha mateso hakiwezi kupita mbali nami, bila mimi kukikunywa, basi mapenzi yako yafanyike!”
Kwa wakati ule Petro na wenzake walikuwa wamewezwa sana na usingizi; lakini wakaamuka, wakaona ule utukufu wa Yesu na wale watu wawili waliokuwa wakisimama pamoja naye.
Kijana mumoja, aliyeitwa Eutiko, alikuwa akiikaa kwenye dirisha. Na kwa muda ule murefu Paulo alipofundisha, Eutiko akaanza kusinziasinzia na kwa mwisho akawezwa na usingizi na akaanguka chini toka kwenye gorofi ya tatu. Walipomunyanyua alikuwa amekwisha kufa.