Nyoka alikuwa mwerevu kuliko nyama wote wa pori walioumbwa na Yawe Mungu. Basi, nyoka akamwambia yule mwanamuke: “Ni kweli Mungu alisema musikule matunda ya muti wowote katika bustani?”
Kulikuwa kumebaki siku mbili mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka na ya Mukate Usiyotiwa Chachu. Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria walitafuta njia ya kumukamata Yesu kwa werevu kusudi wamwue.
na kusema: “Wewe mutoto wa Shetani unayejaa udanganyifu na ukorofi wa kila namna! Wewe usiyependa kuona jambo la haki! Wewe hauchoki na kugeuza maneno ya ukweli ya Bwana!
Lakini ninaogopa kwamba sawa vile nyoka alivyomudanganya Eva kwa werevu wake, mawazo yenu vilevile yasipotoshwe hata mupate kupoteza uaminifu na ukamilifu wenu kwa Kristo.