Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 26:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wakubwa wa makuhani na wasimamizi wa watu wakakusanyika ndani ya nyumba ya Kuhani Mukubwa, aliyeitwa Kayafa,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 26:3
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Muchana kutwa wanatunga maneno juu yangu; mawazo yao yote ni ya kunizuru.


Nami nilikuwa kama kondoo mupole anayepelekwa kuchinjwa; sikujua kwamba shauri walilofanya lilikuwa juu yangu. Wao walisema: Tuuharibu muti pamoja na matunda yake, tumwue apate kusahaulika katika dunia, jina lake lisikumbukwe tena.


Lakini musiponisikiliza na mukiacha kuihesabu siku ya Sabato kama siku takatifu, musipoacha kubeba mizigo na kuingia nayo kupitia milango ya Yerusalema siku ya Sabato, basi nitawakisha moto katika milango yake, nao utateketeza nyumba zote nzuri za Yerusalema, wala hautazimika. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wakati ule Petro alikuwa akiikaa inje katika kiwanja. Mutumishi mumoja mwanamuke akamufikia na kumwambia: “Wewe vilevile ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”


Kisha waaskari wa liwali Pilato wakamupeleka Yesu ndani ya upango wa nyumba ya liwali, nalo kundi lao lote wakakusanyika na kumuzunguka.


Petro akamufuata Yesu kwa mbali, hata akaingia ndani ya upango wa nyumba ya Kuhani Mukubwa. Pale akaikaa pamoja na walinzi, akiota moto.


Petro alipokuwa angali chini ndani ya upango, mumoja wa watumishi wanawake wa Kuhani Mukubwa akafika pale.


Waaskari wakamupeleka Yesu ndani ya upango wa nyumba ya liwali, nao wakaita kundi lao lote wakusanyike.


Wakakonga moto katikati ya kiwanja na kuikaa, na Petro akakuja kuota moto pamoja nao.


nao Anasi na Kayafa walikuwa Makuhani Wakubwa. Halafu Mungu akatoa ujumbe wake kwa Yoane mwana wa Zakaria katika jangwa.


Nao wakubwa wa makuhani na Wafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mutu akijua pahali Yesu alipokuwa, alete habari kusudi wapate kumufunga.


Kisha Anasi akamutuma Yesu, akiwa amefungwa, kwa Kayafa Kuhani Mukubwa.


Na kulipokucha asubui mapema, wakamutosha Yesu kwa Kayafa na kumupeleka kwenye nyumba ya liwali. Lakini Wayuda wenyewe hawakuingia ndani ya nyumba ya liwali, kwa maana kwa njia ile wangejichafua na kutoweza kuwa tayari kula karamu ya Pasaka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ