Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 26:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Mwana wa Mutu atakufa sawa vile Maandiko Matakatifu yanavyosema juu yake, lakini ole kwa mutu yule atakayemutoa! Ingekuwa heri kwake kama asingezaliwa!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 26:24
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”


Sisi tulizoea kuzungumuza kirafiki; pamoja tulikwenda katika nyumba ya Mungu.


Utue muzigo wako kwa Yawe, naye atakusaidia; hamwachilii mutu wa haki ashindwe.


Kisha majuma hayo makumi saba na mawili, yule aliyepakwa mafuta atauawa na hatabaki na kitu. Muji na Pahali Patakatifu Sana vitaharibishwa na waaskari wa mutawala atakayekuja kushambulia. Mwisho wake utafika kama mafuriko, kukiwa vita na maangamizi kama yalivyopangwa na Mungu.


Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


Ole kwa dunia kwa ajili ya vikwazo vinavyokuwa ndani yake! Vikwazo haviwezi kosa kutokea, lakini ole kwa mutu yule anayevileta!


Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Usiku huu ninyi wote mutaanguka kwa ajili yangu, kwa maana imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: ‘Nitamwua muchungaji, na kondoo wa kundi watasambazwa.’


Lakini namna gani yangetimia Maandiko Matakatifu yanayosema kwamba mambo haya yanapaswa kuwa hivi?”


Mambo haya yote yamefanyika kusudi maneno yanayosemwa na manabii katika Maandiko Matakatifu yapate kutimia.” Basi wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.


Kwa maana Mwana wa Mutu atakufa sawa vile Maandiko Matakatifu yanavyosema juu yake, lakini ole kwa yule mutu atakayemutoa! Ingekuwa heri kwake kama asingezaliwa.”


Yesu akawajibu: “Hakika Elia anapaswa kurudi kwanza kutengeneza mambo yote. Lakini sababu gani Maandiko Matakatifu yanasema vilevile kwamba Mwana wa Mutu atateswa sana na kuzarauliwa?


Kwa maana Mwana wa Mutu atakufa sawa vile ilivyokusudiwa na Mungu; lakini ole kwa mutu yule atakayemutoa!”


akiwaambia: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu kwamba Kristo atateswa na kufufuka kwa siku ya tatu kisha kufa kwake.


Wakati nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda kwa uwezo wa jina lako, ndilo lile jina ulilonipa. Nimewachunga wala hakuna mumoja wao aliyepotea, isipokuwa yule anayepaswa kupotea, kusudi Maandiko Matakatifu yatimizwe.


Waaskari wakaambiana: “Tusipasue kanzu hii, lakini tuipigie kura, kusudi tujue itakuwa ya nani.” Mambo haya yalifanyika kusudi Maandiko Matakatifu yanayosema hivi yatimie: “Waligawanya nguo zangu nayo kanzu yangu wakaipigia kura.” Mambo hayo ndiyo waaskari waliyofanya.


Kisha, Yesu akiwa anajua kwamba mambo yote yametimia, akasema hivi kusudi Maandiko Matakatifu yatimie: “Ninasikia kiu.”


Mutu huyu alitolewa kwenu kufuatana na mupango uliokusudiwa na kujulikana na Mungu tangu zamani. Nanyi mulimwua, kwa kumutia katika mikono ya wenye zambi wamutundike juu ya musalaba.


Halafu wakapanga siku ya kukutana na Paulo. Na siku ile watu wengi zaidi wakamufikia pahali alipopanga. Na tangu asubui mpaka magaribi Paulo akawaelezea mambo mengi na kutoa ushuhuda juu ya habari za Ufalme wa Mungu. Alitaka wasadiki habari za Yesu akitaja maneno ya Sheria ya Musa na ya vitabu vya manabii.


Hivi walitimiza mambo uliyokuwa umekusudia tangu zamani kwa uwezo wako na kwa mapenzi yako.


Kwanza nimewatolea mafundisho haya ambayo mimi mwenyewe nilipokea: Kristo alikufa kwa sababu ya zambi zetu kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ