23 Yesu akajibu: “Yule aliyechovya mukate pamoja nami ndani ya sahani ndiye atanitoa.
Wanasema: “Magonjwa haya yatamwua; hatatoka tena ndani ya kitanda chake!”
Muvivu anatia mukono wake katika sahani lakini hauinui mpaka kwenye midomo.
Wanafunzi wakahuzunika sana na kuanza kumwuliza mumoja kwa mumoja: “Bwana, ni mimi?”
“Lakini muangalie: yule anayenitoa anachangia chakula pamoja nami.
“Sisemi juu ya ninyi wote; ninawajua wale niliowachagua. Lakini inafaa maneno haya yanayosemwa na Maandiko Matakatifu yatimie: ‘Yule aliyechangia chakula nami, amenigeuka.’