Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 26:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Yesu akawaambia kwamba waende katika muji kwa mutu mumoja na kumwambia: “Mwalimu anasema: ‘Siku yangu inakaribia. Mimi na wanafunzi wangu tutakula karamu ya Pasaka kwako.’ ”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 26:18
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na kama mutu akiwauliza neno, mumwambie kama Bwana yuko na lazima ya kuwatumia. Na mara moja mutu yule atawaruhusu kuwapeleka.”


Musikubali kuitwa ‘Waongozi,’ kwa maana muko na Mwongozi Mukubwa mumoja tu, ndiye Kristo.


Lakini ninyi musikubali kuitwa ‘Mwalimu’, kwa maana ninyi wote ni wandugu, nanyi muko na Mwalimu mumoja tu.


Nao wanafunzi wakafanya sawa Yesu alivyowaagiza, wakatayarisha karamu ya Pasaka.


“Munajua kwamba kumebaki siku mbili mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mutu apate kutolewa kusudi atundikwe juu ya musalaba.”


Yuda alipofika, akamujongelea Yesu, na kumwambia: “Jambo, Mwalimu.” Na kisha akamubusu.


Yesu alipokuwa hajamaliza kusema maneno haya, wajumbe wakafika kutoka kwa yule mukubwa wa nyumba ya kuabudia na kumwambia: “Binti yako amekwisha kufa. Basi kwa sababu gani ungali unamusumbua Mwalimu?”


Siku zote nilipokuwa pamoja nanyi katika hekalu, ninyi hamukunikamata. Lakini hii ni saa yenu; saa ya utawala wa bwana wa giza.”


Marta alipokwisha kusema maneno hayo, akaenda kumwita dada yake Maria na kumwambia kwa siri: “Mwalimu amekuja, na anakuita.”


Yesu akawajibu: “Saa ya kutukuzwa kwa Mwana wa Mutu imetimia.


Kulikuwa kumebaki siku moja mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kutoka katika dunia na kurudi kwa Baba yake imetimia. Yeye alikuwa akiwapenda watu wake waliokuwa katika dunia, na akaendelea kuwapenda mpaka mwisho.


Wakati Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akainua macho mbinguni na kusema: “Baba, wakati umetimia. Uonyeshe utukufu wa Mwana wako, kusudi Mwana wako aonyeshe utukufu wako vilevile.


Yesu akamwambia: “Maria!” Naye akageuka, akasema kwa kiebrania: “Raboni,” maana yake “Mwalimu.”


Basi wakatafuta kumufunga, lakini hakuna mutu aliyemukamata, kwa sababu saa yake ilikuwa haijatimia.


Na Yesu akawaambia: “Wakati unaofaa kwangu haujatimia; lakini wakati wowote unafaa kwenu.


Ninyi muende kwa sikukuu. Mimi sijaenda bado kwa sikukuu hii, kwa sababu wakati unaofaa kwangu haujatimia.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ