Halafu, bila kujua kwamba huyo alikuwa muke wa mwana wake, akamwendea pale kando ya njia, akamwambia: “Ninataka kulala nawe.” Tamari akamwuliza: “Utanipa nini upate kulala nami?”
Kama ngombe yule akimupiga pembe mutumwa au mujakazi, mwenye ngombe atamulipa bwana wa yule mutumwa feza zenye bei ya shekeli makumi tatu na yule ngombe anapaswa kuuawa kwa kupigwa mawe.
Hao ni kama imbwa walafi sana, wala hawawezi kutosheka hata kidogo. Wachungaji nao hawana akili yoyote. Kila mumoja anatafuta njia yake mwenyewe, kila mumoja anatafuta faida yake.
(Yuda alinunua shamba kwa njia ya feza alizopata kwa ajili ya kitendo chake cha uovu. Pale akaangukia kichwa chini, maiti yakapasuka na matumbotumbo yake yote yakatoka inje.
Na kwa sababu ya tamaa yao mbaya ya mali, walimu hawa wa uongo watajipatia faida juu yenu kwa njia ya maneno ya uongo. Lakini tangia zamani hukumu yao imekwisha kutangazwa, nao hawatakawia kuangamizwa.
Wakubwa wa Wafilistini wakamwendea Delila, wakamwambia: “Umubembeleze Samusoni kusudi ujue asili ya nguvu zake nyingi kusudi tuweze kumukamata na kumufunga. Ukifanya hivyo, kila mumoja wetu atakupa vikoroti makumi tatu vya feza.”
Mika akamwambia: “Kaa pamoja nami, ukuwe kwangu kama baba na kuhani wangu. Nitakulipa vikoroti kumi vya feza kila mwaka na nguo pamoja na mahitaji yako.”