Yesu alipokuwa hajamaliza kusema, Yuda, mumoja wa wanafunzi kumi na wawili, akafika pamoja na kundi kubwa la watu wenye panga na magongo. Hawa wote walikuwa wametumwa na wakubwa wa makuhani na wasimamizi wa watu.
Basi Yuda, aliyemutoa Yesu, alipoona kwamba Yesu amekwisha kuhukumiwa, akajuta, akawarudishia wakubwa wa makuhani na wasimamizi wa watu vile vikoroti makumi tatu vya feza.
Wakati Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakikula chakula cha magaribi, Shetani alikuwa amekwisha kumushawishi Yuda mwana wa Simoni Iskariota kwamba amutoe Yesu.
Yesu akajibu: “Nitachovya kipande cha mukate. Yule nitakayemupa kipande kile ndiye yeye.” Basi Yesu akachovya kipande cha mukate na kumupa Yuda mwana wa Simoni Iskariota.
“Wandugu zangu, ilikuwa lazima yale Maandiko Matakatifu yatimie ambayo Roho Mutakatifu alitabiri kwa kinywa cha mufalme Daudi juu ya Yuda, yule aliyewaongoza wale waliomukamata Yesu.
(Yuda alinunua shamba kwa njia ya feza alizopata kwa ajili ya kitendo chake cha uovu. Pale akaangukia kichwa chini, maiti yakapasuka na matumbotumbo yake yote yakatoka inje.