18 Lakini yule aliyepewa furushi moja, akachimba shimo katika udongo na kuficha ile mali ya bwana wake mule.
Mutu muvivu katika kazi yake ni ndugu ya muharibifu.
Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.
Na yule aliyepata furushi mbili akafaidia zingine mbili.
“Kulipopita siku nyingi, bwana wa watumishi wale akarudi, akafanya hesabu ya mali yake pamoja nao.
Kisha mutumishi mwingine akakuja akasema: ‘Bwana, furushi yako ndiyo hii. Niliichunga vizuri nikiifunga ndani ya kitambaa,
Basi musigeuke kuwa wavivu, lakini mufuate mufano wa wale wanaoamini na kuvumilia. Kwa njia hiyo wanapokea yale Mungu aliyoahidi kuwapa.
Kwa maana mukiwa na tabia hizi zote kwa uwingi, zitawawezesha kutumika na kuzaa matunda hata mupate kumujua Bwana wetu Yesu Kristo.