Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 24:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 “Halafu watu watawatoa kusudi muteswe na kuuawa, na watu wa mataifa yote watawachukia ninyi kwa ajili yangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 24:9
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mwovu ni chukizo kwa mwenye haki, naye mwenye haki ni chukizo kwa mwovu.


Wenye hekima kati ya watu watawafundisha wengi. Hata hivyo, kwa siku chache watauawa kwa upanga au kwa moto, watakamatwa mateka au kunyanganywa mali zao.


na wengine wakawakamata wale watumishi wakawatesa na kuwaua.


Kwa sababu hiyo, nitawatumia manabii na watu wenye hekima na walimu. Mutawaua wamoja wao, mutatundika wengine juu ya misalaba, mutawapiga wengine fimbo ndani ya nyumba zenu za kuabudia na kuwafukuza muji kwa muji.


Kwa sababu hii, Mungu anasema katika hekima yake: ‘Nitawatumia manabii na mitume; watawaua wamoja kati yao na kuwatesa wengine wao.’


Lakini mbele mambo hayo yote yatokee, mutakamatwa na kuteswa. Watawapeleka kwenda kuhukumiwa katika nyumba za kuabudia na kuwatia katika vifungo. Vilevile mutapelekwa mbele ya wafalme na ya wakubwa kwa ajili ya jina langu,


“Kama dunia ikiwachukia ninyi, mujue kwamba ilinichukia mimi mbele ya kuwachukia.


Lakini watawafanyia ninyi haya yote kwa ajili yangu, kwa sababu hawamujui yule aliyenituma.


Watawatenga musiingie katika nyumba za kuabudia. Na kutakuwa wakati ambapo wote watakaowaua watazani kwamba wanamutumikia Mungu.


Lakini tungependa kusikia mawazo yako kwa maana tunajua kwamba fasi zote watu wanapinga dini hii unayofuata.”


Walipokuwa wakimutupia mawe, Stefano akaomba akisema: “Ee Bwana Yesu, pokea roho yangu.”


Lakini mutu akiteswa kwa sababu yeye ni mukristo, asione haya, lakini atukuze Mungu kwa kuwa anaitwa kwa jina lile.


Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.


Ninajua pahali pale unapokaa, ile ndiyo nafasi ya utawala wa Shetani. Wewe unashikamana na jina langu, wala haukuikana imani unayokuwa nayo kwangu, hata wakati Antipa, mushuhuda wangu mwaminifu, alipouawa kati yenu kule kwenye makao ya Shetani.


Nami nikamujibu: “Bwana wangu wewe ndiwe unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wanaotoka katika mateso makubwa. Wamesafisha kanzu zao na kuzifanya kuwa nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ