Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 24:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kwa maana taifa litapigana na taifa, na ufalme utapigana na ufalme. Kutakuwa njaa na tetemeko ya inchi katika pahali mbalimbali.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 24:7
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Taifa moja lilipigana na taifa lingine na muji mumoja ulipigana na muji mwingine, kwa sababu Mungu aliwafazaisha kwa taabu za kila aina.


Mimi nitawachonganisha Wamisri wao kwa wao. Ndugu atapigana na ndugu yake, jirani atapigana na jirani yake, muji mumoja na muji mwingine, mufalme mumoja na mufalme mwingine.


Yawe wa majeshi atakuja kukusaidia; atakuja na ngurumo, tetemeko la inchi na sauti kubwa; atakuja na upepo mukali, zoruba na moto wenye kuunguza.


Lakini Bwana wetu Yawe anasema: Tena nitauazibu Yerusalema kwa mapigo yangu mane ya hukumu kali: vita, njaa, nyama wakali na ugonjwa mukali, nipate kuangamiza watu na nyama ndani yake!


Mushale ulioangukia kwa upande wa mukono wake wa kuume, ulionyesha Yerusalema. Pale wataweka vifaa vya vita kwa kuubomoa. Anaamuru mauaji, kelele za vita zipigwe, vifaa vya vita kwa kubomoa milango viwekwe, lundo ya udongo na minara kwa kuushambulia muji viwekwe vilevile.


Siku ile, hofu kutoka kwa Yawe itawapata watu, na kila mutu atamushambulia mwenzake.


Kutakuwa tetemeko kubwa la inchi. Vilevile kutakuwa njaa na magonjwa makali kwenye nafasi mbalimbali. Zaidi ya ile kutakuwa mambo ya kuogopesha na vitambulisho vya ajabu toka mbinguni.


Na mumoja wao, aliyeitwa Agabo, akasimama, akatabiri kwa njia ya Roho Mutakatifu kwamba kutakuwa njaa kubwa katika dunia nzima. (Nayo ikatokea katika nyakati za utawala wa mufalme Klaudio wa Roma.)


Nami nitafanya maajabu juu katika mbingu na vitambulisho chini katika dunia: kutakuwa damu, moto na moshi mwingi.


Neno hili “mara moja tena” linaonyesha kwamba vitu vilivyoumbwa vitatikiswa na kutoweka, kusudi vile visivyoweza kutikiswa vipate kudumu.


Kisha nikaona mambo haya: Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa sita, kukakuwa tetemeko kubwa la dunia; jua ikageuka kuwa nyeusi kama nguo ya kilio na mwezi ukageuka kuwa mwekundu kama damu.


Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa tatu, nikasikia kiumbe cha tatu cha ajabu kikisema: “Kuja!” Niliangalia nami nikaona farasi mweusi. Na yule aliyepanda juu yake alikuwa na mizani katika mikono yake.


Nikasikia kitu kama sauti iliyotokea katikati ya vile viumbe vine vya ajabu ikisema: “Kilo moja ya ngano ni mushahara wa siku nzima ya kazi, na kilo tatu ya shayiri ni mushahara wa siku nzima ya kazi, lakini usiharibu mafuta wala divai.”


Nikaangalia, nami nikaona farasi mwenye rangi ya kijivujivu. Na yule aliyepanda juu yake aliitwa Lufu, naye alikuwa akisindikizwa na Kuzimu. Wao wakapewa uwezo juu ya sehemu moja ya ine ya dunia kwa kuua watu kwa upanga, kwa njaa kubwa, kwa ugonjwa mukali na kwa nyama wakali.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ