Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 24:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Mutasikia habari za matokeo au utetezi wa vita, lakini musiogope. Sherti mambo hayo yatukie, lakini hayaonyeshi kama mwisho umefika.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 24:6
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Haogopi habari mbaya; moyo wake unasimama imara na anamutegemea Yawe.


Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.


Umwambie akuwe macho, atulie na asiogope wala asivunjike moyo, kwa sababu ya hasira kali ya mufalme Resini wa Aramu, na ya mwana wa Remalia. Hao wawili ni kama tu moshi wa kuni zinazozimika.


Ee upanga wa Yawe! Utatwaa muda gani ndipo utulie? Ingia katika mufuko wako, upate kutulia na kunyamaza!


Lakini watu wa Yerusalema watauzania kuwa ni utabiri wa uongo kwa sababu ya mapatano waliyofanya. Hata hivyo unabii huu utawakumbusha uovu wao na kusababisha kukamatwa kwao.


Mufalme Herode aliposikia maneno haya, akafazaika sana pamoja na wakaaji wote wa Yerusalema.


Na hii Habari Njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia nzima kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; na halafu mwisho wa dunia utatimia.


Lakini namna gani yangetimia Maandiko Matakatifu yanayosema kwamba mambo haya yanapaswa kuwa hivi?”


Lakini muendelee kuvumilia, maana kwa njia ile mutaokoa uzima wenu.”


Musiogope wakati mutakaposikia habari za vita na za mapinduzi. Sherti mambo hayo yatukie kwanza, lakini haionyeshi kwamba mwisho wa dunia unatimia palepale.”


Kwa maana ninawaambia, ni lazima yatimie kwangu maneno haya yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Naye alihesabiwa pamoja na watenda maovu.’ Kwa sababu yanayonielekea mimi yanafikia kwa mwisho wake.”


Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Musifazaike; mumwamini Mungu, na muniamini mimi vilevile.


“Ninawaachia amani; ninawapa amani yangu. Siwapatii ninyi amani hii kama dunia inavyoitoa. Musifazaike wala musiogope.


musifazaike upesi wala kuogopa kwamba Siku ya kurudi kwa Bwana imekwisha kutimia. Inawezekana munafahamu mambo yale kwa njia ya unabii, mahubiri na barua inayosemeka kwamba imetoka kwetu.


Kisha kukatokea farasi mwengine mwekundu. Na yule aliyepanda juu yake akapewa uwezo wa kuondoa amani katika dunia, kusudi watu wauane wao kwa wao. Naye akapewa upanga mukubwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ