Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 24:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Watu wengi watakuja wakijiita kwa jina langu, wakisema: ‘Mimi ni Kristo!’ Nao watawadanganya wengi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 24:5
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye Yawe akaniambia: Hao manabii wanatoa unabii wa uongo kwa jina langu. Mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru, wala sikusema nao. Wanawatabiria maono ya uongo, maaguzi yao hayana maana yoyote, wao wanajitungia uongo wenyewe.


Yawe anaendelea kusema: Mimi sikuwatuma hao manabii, lakini wao walikwenda mbio; sikuwaambia kitu chochote, lakini wao walitabiri!


Mimi nimeyasikia maneno waliyosema hao manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema: Nimeota ndoto, nimeota ndoto!


Yawe anasema hivi: Musijidanganye wenyewe na kusema kwamba waaskari wa Wakaldea wataondoka. Kweli hawataondoka.


Manabii wengi wa uongo watatokea, nao watawadanganya watu wengi.


kwa maana kutatokea watu wanaojiita kwa uongo ‘Kristo’ pamoja na manabii wa uongo, nao wataonyesha vitambulisho vikubwa na maajabu, hata ikiwezekana, wawadanganye hata watu waliochaguliwa na Mungu.


Mimi nimekuja kwa jina la Baba yangu, nanyi hamutaki kunipokea. Lakini ikiwa mwingine anakuja kwa jina lake mwenyewe, ninyi mutamupokea.


Ni kwa sababu hii niliwaambia ninyi kama mutakufa katika zambi zenu. Musipoamini kwamba ‘Mimi Ndimi’, hakika mutakufa katika zambi zenu.”


Halafu Yesu akawaambia: “Wakati mutakapomunyanyua Mwana wa Mutu juu, mutafahamu kwamba ‘Mimi Ndimi.’ Na zaidi ya hii mutatambua kwamba sifanyi neno lolote kwa mapenzi yangu, lakini ninasema tu yale niliyofundishwa na Baba.


Watoto wangu, huu ni wakati wa mwisho. Mulisikia habari kwamba mupinga Kristo atakuja, lakini hata sasa wapinga Kristo wengi wametokea. Na kwa hiyo tunajua kwamba ni wakati wa mwisho.


Ni nani anayekuwa musema uongo? Ni yule anayekana kwamba Yesu si Kristo. Huyu ndiye mupinga Kristo, kwa maana anamukana Baba na Mwana.


Lakini mutu yeyote asiyemusadikia Yesu hana Roho anayetoka kwa Mungu. Mutu yule yuko na roho ya mupinga Kristo. Ninyi mumekwisha kusikia kwamba roho yule atakuja, na sasa amekwisha kuja katika dunia.


Wakaaji wote wa dunia watamwabudu, ndio wale wote ambao tangia kuumbwa kwa dunia, majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ