44 Kwa hiyo, ninyi vilevile mukuwe tayari, kwa sababu Mwana wa Mutu atarudi saa musiyozania.
Kwa maana kama vile umeme unavyoangaza na kuonekana katika mbingu yote, ni vile Mwana wa Mutu atakavyoonekana siku atakapokuja.
Basi mukeshe, kwa sababu hamujui siku Bwana wenu atakaporudi.
Munajua vema kwamba mwenye nyumba angalijua wakati gani mwizi atakapokuja kuiba, angalikesha na kuchunga nyumba yake isibomolewe.
Wale wajinga walipokwenda kununua mafuta, bwana-arusi akafika. Wale wenzao watano waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika karamu ya ndoa. Kisha mulango ukafungwa.
Na Yesu akaongeza kusema: “Basi mukeshe, kwa sababu hamujui siku wala saa ile.
Munajua vema kwamba mwenye nyumba angejua saa gani mwizi atakapokuja kumwiba, asingeacha nyumba yake ibomolewe.
Kwa hiyo ninyi vilevile mukuwe tayari, kwa sababu Mwana wa Mutu atarudia saa musiyozania.”
Basi mukeshe na kuomba kila wakati, kusudi mupate nguvu ya kuepuka mambo hayo yote yatakayotokea, nanyi mupate kuweza kusimama mbele ya Mwana wa Mutu.”
Muonyeshe upole wenu kwa watu wote, kwa maana Bwana yuko karibu kurudia.
Wandugu zangu, musinungunikiane ninyi kwa ninyi kusudi Mungu asiwahukumu. Muangalie, mwamuzi ni karibu, naye amekuwa kwenye mulango!
Tufurahi na kushangilia na kumutukuza, kwa sababu saa ya ndoa ya Mwana-Kondoo imetimia, naye bibi arusi wake amejitayarisha.”