Matayo 24:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
29 “Mara moja kisha mateso ya siku zile, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka toka mbinguni na vyote vyenye nguvu katika mbingu vitatikiswa.
Kisha mwezi utafezeheka, nalo jua litapata haya ya kuangaza, maana Yawe wa majeshi atatawala kule Yerusalema katika mulima Sayuni; ataonyesha wazee wa watu wake utukufu wake.
Siku Bwana atakaporudi, itatimia kama vile mwizi anavyokuja. Siku ile mbingu zitatoweka kwa shindo kubwa, na viumbe vyote vinavyoangaza katika mbingu vitayeyuka. Dunia na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake vitateketezwa.
Kisha malaika wa ine akapiga baragumu. Sehemu moja ya tatu ya jua ikaharibishwa pamoja na sehemu moja ya tatu ya mwezi na ya nyota. Sehemu zile tatu zikaingiwa na giza. Hivi hakukuwa mwangaza kwa muda wa sehemu moja ya tatu ya saa za muchana na sehemu moja ya tatu ya saa za usiku vilevile.