Matayo 24:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
22 Na kama Mungu asingepunguza siku zile za mateso, hakuna hata mutu mumoja angeponyoka kufa. Lakini kwa ajili ya watu wake aliowachagua, yeye atazipunguza.
Hata kukibaki sehemu moja ya kumi ya watu, nao vilevile watateketezwa. Hao watakuwa kama muti wa muvinje au wa mwalo ambao shina lake limebaki kisha kukatwa. Shina hilo ni mbegu takatifu ya mwanzo mupya.
Yawe atayakusanya mataifa yote kwa kuushambulia Yerusalema. Muji utakamatwa, nyumba zenu zitatekwa, na wanawake wenu watakamatwa kwa kinguvu. Nusu ya wakaaji wa muji watapelekwa katika uhamisho, lakini nusu itakayobaki haitaondoshwa inje ya muji.
kwa maana kutatokea watu wanaojiita kwa uongo ‘Kristo’ pamoja na manabii wa uongo, nao wataonyesha vitambulisho vikubwa na maajabu, hata ikiwezekana, wawadanganye hata watu waliochaguliwa na Mungu.
Baragumu kubwa itapigwa, halafu atawatuma wamalaika wake katika pande ine za dunia, kusudi wawakusanye watu wake aliowachagua, kutoka katika dunia nzima.
Na kama Bwana asingepunguza siku zile za mateso, hakuna hata mutu mumoja ambaye angeponyoka kufa. Lakini kwa ajili ya wachaguliwa aliowachagua amezipunguza.
Watoto wale walipokuwa hawajazaliwa bado, wala hawajatenda jambo lolote zuri au baya, Mungu alimwambia Rebeka hivi juu yao: “Mukubwa atamutumikia mudogo.” Alisema vile kwa kutimiza mupango wake unaotokana na uchaguzi wake usiofuatana na matendo ya watu, lakini mwito wake kwao.
Ni kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya watu ambao Mungu alijichagulia kuwa wake, kusudi wao vilevile wapate kuokoka na kupata utukufu wa milele unaopatikana kwa njia ya Kristo Yesu.
Barua hii inatoka kwangu mimi Petro, mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi muliochaguliwa na Mungu na ambao mulisambazwa, na munaoishi kama wakimbizi kule Ponto, Galatia, Kapadokia, Azia na Bitinia.