20 Mumwombe Mungu kusudi kukimbia kwenu kusikuwe wakati wa mvua au kwa siku ya Sabato!
Mufahamu kwamba mimi Yawe nimewapa siku ya Sabato, ndiyo maana nimewapa chakula cha siku mbili kwa siku ya sita. Basi, kila mutu apumzike ndani ya nyumba yake. Mutu yeyote asitoke katika siku ya saba.”
Wanawake wenye mimba na wenye kunyonyesha watapata hasara katika siku zile!
Kwa maana katika siku zile kutakuwa mateso makubwa yasiyotokea tangia kuumbwa kwa dunia mpaka sasa, wala hakutatokea tena mateso kama yale.
Kisha mitume wakarudi Yerusalema tokea kwenye mulima wa Mizeituni unaokuwa karibu na muji huo kwenye umbali wa yapata kilometre moja.