Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 23:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Kwa sababu hiyo, nitawatumia manabii na watu wenye hekima na walimu. Mutawaua wamoja wao, mutatundika wengine juu ya misalaba, mutawapiga wengine fimbo ndani ya nyumba zenu za kuabudia na kuwafukuza muji kwa muji.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 23:34
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yawe akasema kupitia kwa watumishi wake manabii:


Lakini wakamufanyia shauri baya; na kwa amri ya mufalme, wakamupiga mawe kwenye kiwanja cha nyumba ya Yawe.


Tunda la mwenye haki ni muti wa uzima, na mwenye hekima anavuta watu.


Basi Yeremia alipomaliza kutangaza mambo yote ambayo Yawe aliyomwamuru kutangaza kwa watu wote, makuhani, manabii na watu wote walimukamata na kusema: Wewe unapaswa kuuawa!


Mufalme alimwamuru mwana wake Yerameli, Seraya mwana wa Azirieli na Selemia mwana wa Abudieli, wamukamate katibu Baruku na nabii Yeremia. Lakini Yawe aliwaficha.


Watakapowatesa katika muji mumoja, mukimbilie katika muji mwingine. Kweli ninawaambia: hamutamaliza kuzunguka katika miji yote ya Israeli mbele ya kurudi kwa Mwana wa Mutu.


Kisha akawaambia: “Basi, kila mwalimu wa Sheria aliyefundishwa katika Ufalme wa mbinguni, anafanana na mwenye nyumba anayetwaa vitu vipya na vitu vya zamani pamoja toka katika akiba yake.”


Hivi munajishuhudia ninyi wenyewe kuwa ninyi ni ukoo wa watu waliowaua manabii.


Iliandikwa vilevile kwamba kwa jina lake watahubiri mataifa yote, kuanzia Yerusalema, kusudi wageuke toka katika zambi na wapate kusamehewa.


Watawatenga musiingie katika nyumba za kuabudia. Na kutakuwa wakati ambapo wote watakaowaua watazani kwamba wanamutumikia Mungu.


Yesu akawaambia tena: “Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma, mimi ninawatuma ninyi vilevile.”


Lakini mutapokea uwezo wakati Roho Mutakatifu atakaposhuka juu yenu. Nanyi mutakuwa washuhuda wangu katika Yerusalema, katika Yudea yote na Samaria na hata katika inchi zote za dunia.”


Katika siku zile, manabii wamoja walifika Antiokia wakitoka Yerusalema.


Akaamuru Yakobo, ndugu ya Yoane, auawe kwa upanga.


Katika kanisa la Antiokia kulikuwa manabii na walimu wamoja. Kati yao kulikuwa Barnaba, Simoni aliyeitwa vilevile Nigeri; Lukio wa Kurene, Saulo na Manaeni, aliyekomaa pamoja na mufalme Herode.


Kisha Wayuda wamoja wakakuja tokea katika muji wa Antiokia na wa Ikonio. Wakashawishi makundi ya watu wajiunge nao. Wakamutupia Paulo mawe na kumukokotea inje ya muji, wakizani kwamba amekwisha kufa.


Na kufuatana na vile Yuda na Sila walivyokuwa manabii, wakawaonya kwa maneno mengi na kuwajenga moyo.


Wajumbe wa baraza wakakubali shauri la Gamalieli. Halafu wakawaita mitume, wakawapiga fimbo na kuamuru wasifundishe tena kwa jina la Yesu. Kisha wakawaacha kwenda.


Ingawa vile, mimi ninatangaza mambo ya hekima kwa watu waliokomaa kiroho. Lakini mambo haya si ya hekima ya kidunia, wala ya watawala wa dunia hii watakaoangamizwa.


Kwa kadiri ya zawadi Mungu aliyonipatia, kama vile fundi wa kujenga mwenye hekima, niliweka musingi. Na sasa, mutu mwingine anajenga juu yake. Lakini inafaa kila mutu aangalie vizuri namna anavyojenga.


Ni kwa hiyo tunamutangaza Kristo kwa watu wote. Tunaonya na kufundisha kila mutu kwa hekima yote, kusudi tuwasaidie watu wote wapate kufikia kuwa wakamilifu katika kuungana kwao na Kristo.


Wanajikaza kutuzuiza tusitangaze Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kusudi wasiokoke. Hivi wanafikilia kwenye hatua ya mwisho ya zambi walizotenda siku zote. Lakini kwa mwisho kasirani ya Mungu imewaangukia.


Wengine waliuawa kwa kutupiwa mawe, wengine walikatwa vipandevipande kwa misumeno, au kuuawa kwa upanga. Walitangatanga wakivaa ngozi za kondoo au za mbuzi, wakiishi katika umasikini, wakiteswa na kutendewa vibaya.


Wakaaji wa dunia watafurahi kwa ajili ya kifo chao na kushangilia. Watatumiana zawadi, kwa maana manabii hawa wawili waliwasumbua sana wakaaji wa dunia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ