30 Nanyi munasema: ‘Kama sisi tungaliishi katika nyakati za babu zetu, hatungalijiunga nao katika shauri la kuwaua manabii.’
Yawe, Mungu wa babu zao, mara kwa mara alituma kwao wajumbe wake maana alikuwa na huruma kwa watu wake na makao yake.
Niliwaazibu ninyi lakini ilikuwa bure, ninyi munakataa maonyo. Muliwateketeza manabii wenu kwa upanga kama simba mwenye uchu.
“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munajenga makaburi ya manabii na kupamba makaburi ya watu waliokuwa wema.
Hivi munajishuhudia ninyi wenyewe kuwa ninyi ni ukoo wa watu waliowaua manabii.
Muangalie mufano wa Waisraeli: wale wanaokula vitu vinavyotolewa sadaka juu ya mazabahu wanaungana na Mungu kwa njia ya sadaka ile.
Kwa hivi, hatuwezi kukata tumaini tunalokuwa nalo kwenu, kwa maana tunajua kwamba kwa kuwa munashiriki katika taabu yetu, munashiriki vilevile katika kufarijiwa kwetu.