Yawe yuko katika hekalu lake takatifu; kiti cha kifalme cha Yawe kiko mbinguni. Kwa macho yake anawachungulia wanadamu, na kujua kila kitu wanachofanya.
Yawe anasema hivi: Mbingu ni kiti changu cha kifalme, dunia ni kiti cha kupumzikishia miguu yangu. Mutanijengea nyumba ya namna gani basi, pahali nitakapoweza kupumzikia?
‘Mbingu ni kiti changu cha kifalme, nayo dunia ni kiti changu cha kupumzishia miguu. Basi ni nyumba gani munayoweza kunijengea? Au ni nafasi gani munaweza kuniwekea makao?