Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.
Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”
Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”