10 Musikubali kuitwa ‘Waongozi,’ kwa maana muko na Mwongozi Mukubwa mumoja tu, ndiye Kristo.
Lakini anayekuwa mukubwa kati yenu sherti akuwe mutumishi wenu.
Lakini ninyi musikubali kuitwa ‘Mwalimu’, kwa maana ninyi wote ni wandugu, nanyi muko na Mwalimu mumoja tu.
Vilevile hapa katika dunia musimwite mutu yeyote ‘Baba’ kwa maana muko na Baba mumoja tu, anayekuwa mbinguni.
Yesu akawaambia kwamba waende katika muji kwa mutu mumoja na kumwambia: “Mwalimu anasema: ‘Siku yangu inakaribia. Mimi na wanafunzi wangu tutakula karamu ya Pasaka kwako.’ ”
Kuna utumishi wa namna mbalimbali, lakini ni Bwana mumoja ndiye wanayemutumikia.