Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 22:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yeye akawatuma watumishi wake kwa kuwaita watu wale walioalikwa kwa karamu, lakini hawakutaka kufika.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 22:3
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wako wakapata makao ndani yake, uliyotayarishia wamasikini kwa uzuri wako.


Bwana wetu Yawe, Mutakatifu wa Israeli anasema hivi: Mukinirudilia na kutulia mutaokolewa; kwa utulivu na kunitumainia mutapata nguvu. Lakini ninyi hamukutaka.


Hamukutaka kusikiliza wala kutega sikio, ingawa Yawe aliwaletea watumishi wake manabii kila wakati.


Niliwapelekea tena na tena watumishi wangu wote, ni kusema manabii wawaambie kila mumoja wenu aachane na mwenendo wake mwovu, abadilishe matendo yake na kuacha kuifuata na kuitumikia miungu mingine. Na kwamba mukifanya hivyo mutakaa katika inchi niliyowapa ninyi na babu zenu. Lakini ninyi hamukunitegea sikio wala hamukunisikiliza.


Lakini kadiri nilivyozidi kuwaita, ndivyo walivyozidi kwenda mbali nami; waliendelea kuyatambikia Mabali, na kuvifukizia ubani sanamu za miungu.


Watu wangu wamekusudia kuniacha mimi, wakiitwa kusimama wapande juu, hakuna hata mumoja anayeweza.


Munyamaze mbele ya Bwana wenu Yawe, maana siku ya Yawe iko karibu. Yawe ametayarisha sadaka, naye amekwisha kutakasa waalikwa wake.


Wakati siku za mavuno zilipotimia, akawatuma watumishi wake kwa wale walimaji kusudi wamupatie sehemu yake ya mavuno.


“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema. Wewe unaua manabii na kuwatupia mawe wale ambao Mungu anakutumia. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!


akisema: “Mugeuke toka zambi zenu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia!”


Yesu akawajibu: “Munafikiri kwamba warafiki za bwana-arusi wanaweza kufanya kilio wakati bwana-arusi angali pamoja nao? Hapana! Lakini kutakuwa siku bwana-arusi atakapoondoshwa kati yao; ni siku zile watafunga kula.


“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema, wewe unayewaua manabii na wajumbe ambao Mungu anakutumia kwa kuwatupia mawe. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!


Ndugu huyu mukubwa akakasirika na kukataa kuingia ndani ya nyumba. Basi baba yake akatoka inje na kumusihi aingie.


Na sasa kwa ngambo ya wale waadui zangu walionikataa mimi kuwa mufalme wao, muwalete hapa na kuwaua mbele yangu.’ ”


lakini ninyi hamutaki kuja kwangu mupate uzima.


Wayuda walipoona lile kundi la watu, wakajaa na wivu sana, nao wakapinga maneno Paulo aliyosema na kumutukana.


Lakini juu ya Waisraeli anasema hivi: “Muchana kutwa ninanyoosha mikono yangu kwa kuita taifa lenye uasi na ubishi.”


Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?


Kwa sababu hii, Kristo ni mupatanishi wa agano jipya. Kwa njia ya kufa kwake aliwakomboa watu toka katika makosa waliyofanya chini ya uongozi wa agano la kwanza, kusudi wale walioalikwa na Mungu wapate kupokea urizi wa milele aliowaahidia.


Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.


Mara moja mutakapoingia katika muji, mutamukuta mbele hajakwenda kwenye nafasi ya ibada kwenye mulima kwa kula. Maana watu hawatakula mpaka kwanza yeye abariki sadaka. Kisha wale walioalikwa watakula. Hivyo muende haraka; mutakutana naye sasa hivi.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ