Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 22:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Wakamwuliza: “Mwalimu, Musa alisema: ‘Mutu akikufa bila kuacha mutoto, ndugu yake anapaswa kumwoa yule mujane na kumuzalia marehemu watoto.’

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 22:24
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yuda akamwambia Tamari, muke wa mwana wake: “Rudi kwa nyumba ya baba yako, ubaki mujane mpaka wakati mwana wangu Sela atakapokomaa.” Yuda hakutaka Sela naye akufe kama vile wandugu zake. Basi, Tamari akarudi kwa nyumba ya baba yake.


Basi, Yuda akamwambia Onani: “Umutwae muke wa ndugu yako marehemu, maana vile ndivyo inavyokupasa kufanya, upate kumuzalia ndugu yako watoto.”


Halafu wakatuma kwake wamoja kati ya wanafunzi wao pamoja na watu wengine wamoja waliojiunga na Herode kumwuliza maneno haya: “Mwalimu, tunajua kuwa wewe ni mutu wa kweli na kwamba unafundisha kwa kweli njia Mungu anayoamuru. Vilevile haushuguliki na mafikiri ya mutu yeyote kwa sababu hauangalii cheo cha mutu.


Basi huku kwetu kulikuwa wandugu saba. Wa kwanza alioa mwanamuke, kisha akakufa bila kuzaa mutoto. Naye akamwachia ndugu yake yule mwanamuke.


“Mwalimu, katika Sheria, ni amri gani inayokuwa kubwa katikati ya zote?”


“Si kila mutu anayeniita ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, lakini yule tu anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.


“Mwalimu, Musa alituamuru: ‘Mutu akiwa na ndugu yake, naye akikufa na kuacha muke wake bila mutoto, yule ndugu yake anapaswa kumwoa yule mujane na kumuzalia ndugu yake marehemu watoto.’


“Mwalimu, Musa alituamuru: Mutu akiwa na ndugu yake, naye akikufa na kuacha muke wake bila mutoto, yule ndugu yake anapaswa kumwoa yule mujane na kumuzalia ndugu yake marehemu watoto.


Sasa, siku wafu watakapofufuka, muke yule atakuwa wa nani, kwa maana wote saba walikuwa wamemwoa?”


“Sababu gani munaniita ‘Bwana, Bwana,’ nanyi hamufanyi yale ninayowaamuru?


Naye Naomi akawasihi: “Murudi, wabinti zangu. Kwa nini kunifuata? Munafikiri ninaweza kupata tena watoto watakaokuwa waume zenu?


Kwa hiyo, kaa hapa usiku wote, na kesho asubui tutaona kama atakubali kukutunza au hapana. Ikiwa atakutunza ni vizuri. Kama vile Yawe anavyoishi, akikataa, mimi nitakutunza. Lala hapa mpaka asubui.”


Boazi akasema: “Ni vizuri, lakini ukilinunua hilo shamba kutoka kwa Naomi, ni sherti umutwae vilevile Ruta wa Moabu, mujane ambaye ni jamaa wa marehemu, kusudi shamba hilo libaki katika jamaa ya yule marehemu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ