23 Siku ile ile, Wasadukayo wamoja wakamufikia Yesu. (Watu hawa ndio wanaosema kwamba wafu hawatafufuka.)
Yesu akawaambia: “Muangalie vizuri, mujiepushe na chachu ya Wafarisayo na Wasadukayo.”
Yoane alipoona Wafarisayo wengi na Wasadukayo wakimufikia kwa kubatizwa, aliwaambia: “Ninyi kikundi cha nyoka! Ni nani aliyewaambia kwamba munaweza kuponyoka azabu ya Mungu inayokaribia?
Petro na Yoane walipokuwa wangali wakisema mbele ya watu, makuhani, mukubwa wa walinzi wa hekalu pamoja na Wasadukayo wakafika.
Halafu Kuhani Mukubwa na washiriki wake wote, ndio watu wa chama cha Wasadukayo, wakawaonea mitume wivu.
Hao wamepotoka mbali na ukweli, wamepotosha imani ya watu wengi wakisema kwamba ufufuko tunaongojea umekwisha kufanyika.