Petro akawajibu: “Ndiyo, analipa.” Petro alipoingia ndani ya nyumba, mbele hajasema kitu Yesu akamwuliza: “Simoni, unafikiri nini? Wafalme wa dunia wanawalipisha watu gani kodi au malipo mengine mbalimbali? Ni watu wa jamaa zao wenyewe au watu wengine?”
“Mutumishi yule alipoondoka, akakutana na mumoja wa watumishi wenzake aliyekuwa na deni lake la vikoroti mia moja vya feza. Akamukamata na kumunyonganyonga shingo na kumulazimisha kulipa deni lake.
Nikasikia kitu kama sauti iliyotokea katikati ya vile viumbe vine vya ajabu ikisema: “Kilo moja ya ngano ni mushahara wa siku nzima ya kazi, na kilo tatu ya shayiri ni mushahara wa siku nzima ya kazi, lakini usiharibu mafuta wala divai.”