Tungependa ufahamu, ewe mufalme, kwamba muji huu ukijengwa upya na kuta zake zikimalizika, watu hawatalipa kodi, malipo ya kuvuka mipaka, na mengine mbalimbali na hazina yako itapunguka.
Tunawafahamisha tena kwamba inakatazwa kuwadai kodi ya mapato, malipo ya kuvuka mupaka na mengine makuhani, Walawi, waimbaji, walinzi wa mulango, wafanyakazi au watumishi wengine wa nyumba hii ya Mungu.
Kwa sababu ya zambi zetu, utajiri wa inchi hii unawaendea wafalme uliowaleta kwa kututawala. Wanatutawala jinsi wanavyopenda hata na nyama wetu wa ufugo wanawatendea jinsi wanavyopenda, tuko katika taabu kubwa sana.
mumepotoka, mumeyahatarisha maisha yenu. Maana mulinituma kwa Yawe, Mungu wenu, mukiniambia: Utuombee kwa Yawe, Mungu wetu kwamba kitu chochote Yawe, Mungu wetu, atakachosema, utuambie, nasi tutatimiza.
Petro akawajibu: “Ndiyo, analipa.” Petro alipoingia ndani ya nyumba, mbele hajasema kitu Yesu akamwuliza: “Simoni, unafikiri nini? Wafalme wa dunia wanawalipisha watu gani kodi au malipo mengine mbalimbali? Ni watu wa jamaa zao wenyewe au watu wengine?”
Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Tiberio mufalme wa Roma, Pontio Pilato alikuwa liwali wa jimbo la Yudea, na Herode alikuwa mutawala wa jimbo la Galilaya na ndugu yake Filipo alikuwa mutawala wa inchi ya Iturea na ya Tarakoniti. Vilevile Lisania alikuwa mutawala wa inchi ya Abilene,
Nyuma yake, katika siku zile walipofanya hesabu ya watu, kulitokea Yuda wa jimbo la Galilaya. Huyo naye aliwavuta watu wengine kwa kumufuata. Lakini yeye vilevile aliuawa na wanafunzi wake wote wakasambazwa.