Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 22:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Halafu mufalme akawaambia watumishi wake: ‘Mumufunge mutu huyu miguu na mikono na kumutupa inje kwenye giza. Kule atalia na kusaga meno.’ ”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 22:13
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu waovu wanaona hayo na kuuzika. Wanasaga meno kwa chuki na kutoweka. Matumaini ya mutu mubaya yanapotea bure.


Mwovu anamufanyia mutu wa haki shauri baya, na kumusagia meno kwa chuki.


Amuka! Amuka! Ujipatie zile nguvu zako, ewe Sayuni! Uvae nguo yako nzuri, ewe Yerusalema, muji mutakatifu. Maana hawataingia tena kwako watu wasiotahiriwa na wachafu.


Akaamuru watu fulani wenye nguvu kabisa kati ya waaskari wake wawafunge Sadiraki, Mesaki na Abedenego na kuwatupa katika ile furu ya moto mukali.


“Hakuna mutu anayeweza kuingia ndani ya nyumba ya mwenye nguvu na kunyanganya vitu vyake, isipokuwa kwanza anamufunga. Na kisha anaweza kunyanganya vitu vyake vyote.


Muviache vyote viwili vikomae pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati ule nitawaambia wavunaji: muongoe kwanza nyasi, nanyi muzilundike kwa mafungu mafungu kwa kuzichoma, na kisha mukusanye ngano na kuweka mavuno ndani ya gala yangu.’ ”


Nao watawatupa ndani ya furu la moto, na mule watalia na kusaga meno.


Na halafu watawatupa watu wabaya ndani ya furu la moto; na mule watalia na kusaga meno.”


Naye atamupiga vikali na atamwazibu sawa na watu wanafiki, akimuweka kwenye nafasi atakapolia na kusaga meno.


Na zaidi ya hii, mumutupe huyu mutumishi asiyekuwa na mafaa inje kwenye giza. Kule atalia na kusaga meno.’


Lakini wale waliopaswa kushiriki katika Ufalme ule watatupwa inje kwenye giza, na kule watalia na kusaga meno.”


Na kule mutalia na kusaga meno, mutakapowaona Abrahamu, Isaka, Yakobo na manabii wote katika Ufalme wa Mungu. Lakini ninyi mutakuwa mumetupwa inje!


Ninakuambia mambo ya kweli: wakati ulipokuwa kijana, ulijivalisha wewe mwenyewe na kwenda pahali ulipotaka. Lakini wakati utakapokuwa muzee, utanyoosha mikono yako na mutu mwingine atakuvalisha na kukupeleka pahali usipotaka.”


Akatufikia, akatwaa mukaba wa Paulo, akajifunga miguu na mikono yake mwenyewe na kusema: “Roho Mutakatifu anasema: ‘Wayuda watamufunga mutu mwenye mukaba huu namna hii kule Yerusalema na kumutoa kwa watu wa mataifa mengine.’ ”


Wajumbe wa Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kumusagia Stefano meno.


Azabu yao itakuwa kuangamizwa kwa milele, na kutengwa mbali na uso wa Bwana na mbali na utukufu wa uwezo wake,


Wale walimu wa uongo ni kama visima visivyokuwa na maji tena, wao ni kama mawingu yanayopeperushwa na upepo; makao yao yametayarishwa kwenye giza nzito.


Kwa maana Mungu hakuwahurumia wale wamalaika waliofanya zambi, lakini aliwatupa katika jehenamu. Wao wanalindwa mule wakifungwa minyororo katika giza nzito wakingojea Siku ile ya hukumu.


Wanafanana na zoruba kubwa ya bahari na matendo yao ya haya yanaonekana kama pofu ya zoruba. Wanafanana vilevile na nyota zinazotangatanga; Mungu amekwisha kuwawekea nafasi katika giza kubwa kwa milele.


Mukumbuke vilevile wamalaika wale waliokosa kulinda vema cheo chao, lakini wakaacha makao yao: Mungu akawaweka katika nafasi ya giza, wakifungwa minyororo ya milele kwa kungojea Siku ile ya hukumu.


Hakuna kitu chochote kichafu kitakachoingia ndani yake, wala yeye anayefanya machukizo na kusema uongo; lakini wale tu ambao majina yao yaliandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ