Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 22:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 “Naye mufalme alipoingia kwa kuwaangalia wale wageni, akamwona mutu mumoja asiyevaa nguo ya karamu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 22:11
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yehu akamwagiza yule aliyesimamia nguo za ibada hivi: “Ondoa nguo na kuwapa watu wote wanaotumikia Bali.” Musimamizi akatoa nguo zile, akawapa.


Amuka! Amuka! Ujipatie zile nguvu zako, ewe Sayuni! Uvae nguo yako nzuri, ewe Yerusalema, muji mutakatifu. Maana hawataingia tena kwako watu wasiotahiriwa na wachafu.


Hakuna hata mumoja anayekuja kukuomba; hakuna anayejishugulisha kukutafuta. Wewe unauficha uso wako mbali nasi, umetuacha tufungwe na maovu yetu.


Wakati huo nitauchunguza Yerusalema kwa taa, nitawaazibu wanaoishi wakitulia kama machicha ya divai, wote ambao wanasema kati yao: Yawe hatafanya kitu: chema au kibaya.


Muviache vyote viwili vikomae pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati ule nitawaambia wavunaji: muongoe kwanza nyasi, nanyi muzilundike kwa mafungu mafungu kwa kuzichoma, na kisha mukusanye ngano na kuweka mavuno ndani ya gala yangu.’ ”


Nao watumishi wakaenda katika barabara, wakakusanya watu wote waliowaona, wabaya na wazuri, na nyumba ya karamu ikajaa na wageni.


Yeye anashika lungo katika mikono yake kwa kupepeta ngano. Atakusanya ngano na kuitia katika gala yake, lakini atateketeza maganda katika moto usiozimika.”


Lakini Bwana Yesu akuwe kama vile silaha munayobeba, musijiachilie kuvutwa na hali yenu ya kimwili hata mutimize tamaa zake.


kuhesabiwa haki na Mungu kunapatikana kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote wanaoamini, kwa maana hakuna tofauti yoyote kati yao,


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Kwa maana, tukisha kuyavaa hatutaonekana tena kuwa uchi.


Hivi, ninyi wote mulioungana na Yesu Kristo, kwa njia ya kubatizwa, ni kama vile mumevaa Kristo.


Mukuwe na hali mupya, inayoumbwa kwa mufano wa Mungu na inayoonekana katika maisha ya haki na utakatifu wa kweli.


“Sikiliza, ninakuja kwa saa isiyozaniwa kama vile mwizi. Heri yule anayekesha na kutunza nguo zake vizuri kusudi asitembee uchi na kujifezehesha mbele ya watu.”


Yule bibi amepewa nguo ya kuvaa iliyofumwa na nyuzi nzuri zenye kungaa. (Nguo ile ni mufano wa matendo ya haki ya watu wa Mungu.)


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


Kwa hiyo ninakushauria kununua kwangu zahabu iliyosafishwa kwa moto, kusudi upate kuwa tajiri. Vilevile ununue nguo nyeupe, upate kuvaa na kufunika uchi wako unaokuletea haya. Tena ununue dawa ya kutia ndani ya macho yako, kusudi upate kuona.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ