Kwa hiyo, Abramu akaondoka kama vile Yawe alivyomwamuru, na Loti akakwenda pamoja naye. Abramu alikuwa na umri wa miaka makumi saba na mitano alipotoka Harani.
Basi, nikafanya kama nilivyoamriwa. Siku hiyo, wakati wa muchana, nikafunga muzigo wangu kama muzigo wa mutu anayekimbia. Magaribi nikatoboa ukuta na giza lilipokuwa likiingia, nikatoka, nikibeba muzigo wangu juu ya mabega, watu wote wakiniona.
“Muwaambie wakaaji wa muji Sayuni: ‘Angalia, mufalme wenu anakuja kwenu. Yeye ni munyenyekevu, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, kitoto cha punda.’ ”
“Ninajuta kwamba nimemufanya Saulo kuwa mufalme. Yeye ameacha kunifuata mimi na hajatimiza amri zangu.” Samweli alikasirika, akamulilia Yawe usiku kucha.