Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 21:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Na kama mutu akiwauliza neno, mumwambie kama Bwana yuko na lazima ya kuwatumia. Na mara moja mutu yule atawaruhusu kuwapeleka.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 21:3
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Ondoka uende katika muji wa Zerepata, karibu na Sidona, ukae kule. Nimemwamuru mujane mumoja akupatie chakula kule.”


Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Kiro mufalme wa Persia, Yawe akatimiza neno alilosema kwa njia ya nabii Yeremia. Yawe akaamusha nia ya Kiro mufalme wa Persia, naye akatoa amri hii katika ufalme wake, vilevile amri hiyo ikatolewa kwa maandiko:


Basi, viongozi wa ukoo za makabila ya Yuda na Benjamina wakaondoka, makuhani na Walawi, na kila mutu ambaye Mungu alimupa moyo wa kwenda kujenga upya nyumba ya Yawe, inayokuwa Yerusalema.


Ezra akasema: “Asifiwe Yawe, Mungu wa babu zetu, ambaye amemupatia mufalme moyo wa kupamba nyumba ya Yawe inayokuwa Yerusalema.


Zaburi ya Daudi. Dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vya Yawe; ulimwengu na wote wanaoishi ndani yake ni mali yake.


akawaambia: “Mwende katika kijiji kinachokuwa mbele yenu. Wakati mutakapofika kule, mara moja mutaona punda amefungwa na mwana-punda akiwa pamoja naye. Muwafungue na kuwaleta.


Mambo hayo yote yalitokea, kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii:


Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa.


Baba anamupenda Mwana wake, naye ameweka vitu vyote kwa mukono wake.


Yeye hahitaji kushugulikiwa na watu, kama vile angekuwa na lazima ya musaada fulani. Kwa maana yeye ndiye anayewapa watu wote pumzi ya uzima, pamoja na vitu vyote wanavyohitaji.


Shukrani kwa Mungu aliyemutia Tito bidii ya kuwasaidia kama vile sisi tunavyokuwa nayo!


Kwa maana munajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ingawa alikuwa tajiri, yeye mwenyewe alijifanya masikini kwa ajili yenu, kusudi mupate kuwa watajiri kwa njia ya umasikini wake.


Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.


Vilevile, Saulo pamoja na wapiganaji hodari ambao zamani Mungu aligusa mioyo yao, alikwenda kwake kule katika muji wa Gibea.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ