Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 21:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kisha akawaacha, akatoka inje ya muji wa Yerusalema, naye akaenda Betania na kulala kule.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 21:17
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi usikilize maonyo, ee Yerusalema. Kama sivyo nitakutupilia mbali; nitakufanya ukuwe jangwa, kuwa pahali pasipokaliwa na mutu.


Hata kama wakilea watoto, sitamwacha hata mumoja wao muzima. Ole kwao, nitakapowaacha peke yao!


Watu wa kizazi kibaya na kinachokosa uaminifu mbele ya Mungu wanataka kuona kitambulisho. Lakini hawataonyeshwa kitambulisho isipokuwa kitambulisho cha nabii Yona.” Kisha Yesu akawaacha na kujiendea.


Yesu alipokuwa Betania katika nyumba ya mutu aliyeitwa Simoni Mukoma,


Yesu na wanafunzi wake wakakaribia kufika Yerusalema, upande wa kijiji cha Betefage na cha Betania, karibu na mulima wa Mizeituni. Yesu akawatuma wawili katika wanafunzi wake,


Yesu akafika Yerusalema na kuingia ndani ya hekalu. Alipokwisha kuangalia vitu vyote pande zote, akaondoka na kwenda Betania pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili, kwa sababu ilikuwa imekwisha kuwa magaribi.


Ilipokuwa magaribi, Yesu na wanafunzi wake wakatoka katika muji ule.


Yesu alikuwa Betania katika nyumba ya mutu aliyeitwa Simoni Mukoma. Walipokuwa wakikula, mwanamuke mumoja akaingia ndani ya nyumba. Alikuwa na chupa la jiwe lenye marasi ya bei kali yaliyotengenezwa na maua ya nardo safi. Kisha akavunja mudomo wa lile chupa na kumimia marasi juu ya kichwa cha Yesu.


Yesu na wanafunzi wake wakaenda peke yao pembeni ya ziwa la Galilaya, na kundi kubwa la watu walimufuata. Watu hawa walitoka Galilaya na Yudea,


Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakisafiri, wakaingia katika kijiji kimoja. Kule mwanamuke mumoja aliyeitwa Marta akamukaribisha ndani ya nyumba yake.


Alipokaribia kufika katika kijiji cha Betefage na cha Betania upande wa mulima wa Mizeituni, Yesu akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake, akiwaambia:


Kisha Yesu akatoka nao katika muji na kwenda karibu na kijiji cha Betania na pale akainua mikono yake juu na kuwabariki.


Kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Lazaro, muzaliwa wa Betania aliyepatwa na ugonjwa. Wadada zake Maria na Marta walikaa katika kijiji kile.


Kati ya kijiji cha Betania na Yerusalema kulikuwa umbali yapata kilometre tatu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ