Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 21:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Yesu akaingia ndani ya hekalu, naye akawafukuza watu wote waliokuwa wakiuzishia na kununulia vitu vyao ndani yake. Akapindua meza za wale waliobadilisha feza na viti vya wachuuzi wa njiwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 21:12
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kila mumoja atakayehesabiwa anapaswa kulipa nusu ya shekeli kulingana na vipimo vya hema la mukutano. Hii ni sadaka yake atakayonitolea.


Ikiwa anamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa ya ndege, basi, ataleta sadaka yake ya hua au kitoto cha njiwa.


Siku za kutakaswa kwake zitakapotimia, ikuwe amepata mutoto mwanaume au mwanamuke, atamuletea kuhani kwenye mulango wa hema la mukutano mwana-kondoo wa mwaka mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na kitoto cha njiwa au hua, kwa ajili ya sadaka ya zambi.


Kama hawezi kutoa mwana-kondoo, basi, ataleta hua wawili au vitoto viwili vya njiwa; mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya zambi. Kuhani atamufanyia mama huyo ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.


Ataleta vilevile hua wawili au vitoto viwili vya njiwa kadiri anavyoweza mumoja atakuwa kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.


Kisha kuhani atatwaa mumoja wa wale hua au njiwa wawili kadiri mutu yule anavyoweza kuleta.


Siku ya nane, anapaswa kuleta hua wawili au vitoto viwili vya njiwa mbele ya Yawe kwenye mulango wa hema la mukutano na kumupatia kuhani.


Siku ya nane atatwaa hua wawili au vitoto viwili vya njiwa na kumuletea kuhani kwenye mulango wa hema la mukutano.


Ikiwa hawezi kutoa hua wawili au vitoto viwili vya njiwa kama vile sadaka yake kwa ajili ya zambi aliyotenda, basi, ataleta unga kilo moja. Lakini hatautia mafuta wala ubani maana ni sadaka kwa ajili ya zambi.


Lakini kama hawezi kutoa mwana-kondoo wa sadaka ya kosa kwa ajili ya zambi aliyotenda, basi atamuletea Yawe hua wawili au vitoto viwili vya njiwa, mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto.


Yesu akafika Yerusalema na kuingia ndani ya hekalu. Alipokwisha kuangalia vitu vyote pande zote, akaondoka na kwenda Betania pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili, kwa sababu ilikuwa imekwisha kuwa magaribi.


Wakatoa vilevile sadaka sawa vile inavyoagizwa katika Sheria ile: “Hua wawili au vitoto viwili vya njiwa.”


Wakati sikukuu ya Pasaka ya Wayuda ilipokaribia, Yesu akaenda Yerusalema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ