Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 21:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Yesu alipoingia Yerusalema, muji wote ukavuma. Watu wakaulizana: “Huyu ni nani?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 21:10
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ni kitu gani kile kinachotoka katika jangwa kama munara wa moshi, kinachotoa harufu ya manemane na ubani, manukato yanayouzishwa na wachuuzi?


Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, anayefika kutoka Bosira na nguo ya madoa mekundu? Ni nani huyo aliyevaa nguo ya utukufu, anatembea kwa nguvu zake kubwa? Ni mimi Yawe ninayetangaza ushindi wangu; nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.


Mufalme Herode aliposikia maneno haya, akafazaika sana pamoja na wakaaji wote wa Yerusalema.


Kundi la watu wakajibu: “Huyu ni nabii Yesu wa Nazareti katika Galilaya.”


Nalo kundi la watu waliomutangulia Yesu na lile la watu waliofuata nyuma yake, wakaanza kulalamika, wakisema: “Usifiwe wewe Mwana wa Daudi! Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana! Mungu asifiwe juu mbinguni!”


“Utuambie ni kwa mamlaka gani unafanya mambo haya, na ni nani aliyekupa mamlaka yale?”


Walimu wa Sheria na Wafarisayo wakaanza kujiuliza: “Ni mutu gani huyu anayemutukana Mungu? Ni nani anayeweza kusamehe zambi, isipokuwa Mungu peke yake?”


Na waalikwa wengine waliokuwa wakikula pamoja na Yesu, wakaanza kujisemesha: “Ni mutu gani huyu anayesamehe zambi?”


Lakini Herode alisema: “Mimi nimeamuru Yoane akatwe kichwa. Basi huyu ninayesikia habari zake ni nani?” Naye akatafuta namna ya kumwona Yesu.


Basi Wayuda wakamwuliza: “Utaonyesha kitambulisho gani kwa kutuhakikishia kwamba uko na haki ya kufanya hivi?”


Naye akauliza: “Wewe ni nani, Bwana?” Na Bwana akajibu: “Mimi ni Yesu unayemutesa.


Halafu wote wawili wakaendelea na safari mpaka Betelehemu. Walipofika kule, watu wote wakashangaa, hata wanawake wakaulizana: “Huyu ni Naomi?”


Samweli akafanya sawa alivyoambiwa na Yawe, akaenda Betelehemu. Wazee wa muji wakatoka kwenda kumupokea wakiwa wanatetemeka, wakamwuliza: “Umekuja kwa amani?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ