Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 20:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Yesu akawasikilia huruma. Akagusa macho yao, na mara moja wakapata kuona, nao wakamufuata.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 20:34
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mbele sijateswa nilikuwa nimepotea, lakini sasa ninashika neno lako.


Nimefaidika kutokana na taabu yangu, maana imeniwezesha kujifunza masharti yako.


Yawe ni mwenye huruma na rehema; yeye hakasiriki upesi, amejaa wema.


Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, naye akawasikilia huruma, akawaponyesha wale waliokuwa wagonjwa kati yao.


Yesu akawaita wanafunzi wake, na kuwaambia: “Ninawasikilia watu hawa huruma, kwa sababu wamekaa nami sasa kwa muda wa siku tatu, nao hawana chakula tena. Nami sitaki kuagana nao pasipo kula, kusudi wasiregee katika njia.”


Nao wakamujibu: “Bwana, tunakuomba utuponyeshe macho.”


Yesu na wanafunzi wake wakakaribia kufika Yerusalema upande wa kijiji cha Betefage, karibu na mulima wa Mizeituni. Yesu akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake,


Yesu akamugusa mukono, naye akapona homa. Halafu mama yule akasimama na kuanza kumushugulikia.


Halafu Yesu akagusa macho yao, akisema: “Ifanyike kwenu sawa vile munavyoaminia.”


Yesu alipoona kundi la watu, aliwasikilia huruma, kwa maana walikuwa wamesumbuka na kuregea, kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.


Basi Yesu akamwondoa yule mutu kati ya kundi, akaenda naye mbali kidogo, akamutia vidole ndani ya masikio, akatema mate na kumugusa ulimi kwa mate yale.


Na pale pale akapata kuona, na kumufuata Yesu akishukuru Mungu. Na watu wote walipoona jambo hili wakamusifu Mungu.


Lakini Yesu akasema: “Mwache, inatosha!” Akagusa sikio la mutu yule, na kumuponyesha.


Bwana alipomwona yule mama, akamusikilia huruma na kumwambia: “Usilie.”


kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Kwa hiyo ilimupasa afanane na wandugu zake katika mambo yote, kusudi apate kuwa Kuhani Mukubwa anayekuwa mwenye huruma na mwaminifu katika kazi yake mbele ya Mungu, na kwa njia hiyo zambi za watu zisamehewe.


Kwa kumaliza, ninyi wote mukuwe na mawazo na nia moja, mupendane kama wandugu waamini, mukuwe wema na wanyenyekevu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ